Ubaguzi wa watu wenye ulemavu nani alaumiwe na nini kifanyike?!

Hongera sana shule direct kwa jitihada zenu za kuokoa maisha ya watoto katika nyanja ya elimu!……Binafsi najiuliza hivi nani wakulaumiwa na nini kifanyike juu ya watu wenye ulemavu?! Mimi nasema ni ubaguzi wa wazi wazi kwa watu hawa na jamii imelifumbia macho! …….Miaka ya nyuma tulisema kuwa watu hawana uwelewa na leo hii je tunasemaje?! Shule moja ya secondary ya viziwi tena ni private?! Majengo mengi yanajengwa bila kujali kuwa tunao walemavu katika jamii yetu!! Majengo na maeneo mengi hakuna parking za magari specific kwa walemavu! Makanisa mengi sana hayana wakalimani wa viziwi! n.k………Huu ubaguzi ni mpaka lini? Nani wakulaumiwa? Na nini kifanyike? ……..Tafakari na chukua hatua!

Leave a Reply