A word of wisdom

FB_IMG_1453959427549

Huwezi kumzuia ADUI…….

kukutisha, kujitapa, kukukejeli na kukudhihaki, kujiona yeye ndio bora kuliko wewe………kubwa Simama kwenye nafasi yako. Ukikaa kwenye nafasi yako wote waliokukataa, waliokususa, waliokudhihaki, waliokutusi na waliokuona si lolote si chochote ipo siku watakuunga mkono. Waliokuona hufai kuwa kwenye maisha yao…………………..hao hao watasimulia mambo makuu kuhusu wewe, watakutamani na watakuheshimu. Hata wasipokiri kwa vinywa vyao mioyo yao itakiri na kuthibitisha wewe sio wa kawaida. Kumbuka Ulivyo leo sivyo utakavyokuwa kesho. Nakukumbusha tena Kaa kwenye nafasi yako, ndani yako unayo mambo makubwa ambayo bado hujafanya hata Robo.

FB_IMG_1453959328000

Wewe sio wa kawaida…….mtag na umwambie na mshikaji/shost wako wewe sio wa kawaida…Usilale wewe ndio kwanza kumekucha. Simama kwenye nafasi yako. Je nafasi yako unaijua?????

Kutoka Facebook

FB_IMG_1453998045068Nimependa sana hizi picha za rafiki yangu wa miaka mingi sana toka tupo shule pale Kowak Girls Secondary school iliyopo wilaya ya Rorya, mkowa wa Mara. Hapo ndipo tulikutana na mpaka leo hii zaidi ya miaka 20 bado tu marafiki sana.  Yeye anaishi Geita………..ha! ha! ha! Ngoja niwape story moja hivi ya huyu rafiki yangu ??? kwa mara ya kwanza kusikia mvua inapiga kelele kwenye bati ilikuwa shuleni Kowak! Aliliaje sasa, alikuwa anatetemeka kama mtu mwenye mapepo! Tulikuwa wageni kabisa shule tupo form one akasema hakuwahi kusikia mvua ikifanya hivyo , tukawa tunamshangaa lol! Kumbe toka azaliwe amekulia kwenye nyumba za ghorofa ??marehemu baba yake alikuwa General Manager wa Mwatex hivyo siku zote ameishi kwenye nyumba za shirika. Halafu shule alisoma Nyakaoja, Mwanza ambapo nazo ni ghorofa. Maisha ya watu na experience ni tofauti sana, kile ambacho wewe unaweza kufikiria kuwa ni kitu cha kawaida “normal /simple thing” kumbe kwa mwingine ni miujiza! Lakini bado wote ni binadamu na thamani yetu wote ni sawa kabisa…………Kuna binamu yangu yeye alikuwa anasema anaomba Mungu amjalie apate elimu nzuri na pesa ya kuweza kumjengea mama yake nyumba yenye paa ya “mabati” eti naye aweze sikia sauti ya mvua ikinyesha kama wengine ?? kwani akiwa ndani ya nyumba ya “majani” hasikii wala hajui mvua kama inanyesha mpaka atoke nje!! Lakini Mungu si Athumani, her wishes came true! Nasasa hivi ni judge mwenye PhD naalipo anza kazi kitu cha kwanza alimjengea mama yake nyumba ya “mabati”!??FB_IMG_1453998006263Prisca umependeza sana. Mbarikiwe wewe na familia yako. Much love ❤❤

Mh. ShyRose Bhanji-Kikazi zaidi

Screenshot_2016-01-27-11-27-43-1Mh. ShyRose Bhanji akiwa ndani ya Bunge la EALA. Napenda sana kumuangalia huyu dada yangu kwani ni mwanamke shujaa sana. Nimekuwa nikimfatilia safari yake katika maswala ya siasa kwa muda mrefu sana. Kwakweli nimejifunza mengi sana toka kwake kama mwanamke. Hakati tamaa, na haogopi kujaribu. Nimfano mzuri sana kwa watu haswa wanawake ambao wanafikiria kupata “shot cut” kwa kuigawa “miili” yao kwaajili ya kufanikisha malengo yao. Screenshot_2016-01-27-11-27-21-1Well, mtu anaweza sema wapo wanawake waliofanikiwa kwa kuigawa miili yao! Sasa ngoja nikwambie hao wanawake ni kama jipu linalovuja usaa halafu wao wakalipangusa kwa nje na kufunga vizuri na bandage bila kutoa “kiini” cha jipu! HAKUNA MAFANIKIO bali ni wamejiweka au kujijengea daraja la utumwa kwa wanaume! Yani siku zote hawatokuwa na amani wala furaha moyoni mwamgu kwani wanajua wako “powerless” hawawezi simama wenyewe bila kutoa miili yao. Na huwa hawafiki mbAli kabisa. Hii ni hata kwa wale wanao pata maendeleo kwa kutumia njia isiyo halali, huwa hawana amani, wala furaha, hata kama anapesa kiasi gani. Hivyo ni bora uangaike kwa jasho lako hata kama ni kwa tabu lakini matunda yake ni matamu sana. Hongera sana dada yangu Mh. ShyRose Bhanji kwa kuwa mfano mzuri kwa jamii yetu. Ubarikiwe sana. (Pichani ni Mh. ShyRose Bhanji, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Dr. Susan Kolimba, na mwingine ni Mbunge wa EALA).

Shout-out to all strong ladies out there!

Screenshot_2016-01-24-21-10-56-1

Hot shot of the day

IMG-20160127-WA0000Hii leo ndio picha yetu ya moto moto! Baba yangu, kaka yangu mkubwa, wifi yangu mkubwa na my nephew  Gabriel.  Wifi yangu yeye anafanya kazi Utegi Technical Enterprises Ltd, hivyo baba yetu ni “top boss” wake. Kwahiyo hapo kuna undugu wa kidamu na ki-business ??  IMG-20160127-WA0001Mambo yakuchangia gari na mumewe (kaka yangu) basi siku nyingine kaka yangu huwa anabanwa na kazi zake hivyo inabidi wifi yangu apande daladala ?? hiyo haikumpendeza boss wake (baba yetu) jana akaamua kum-surprise na “kausafiri” wake ambao hautumii mafuta sana na hivyo nirahisi kwake kumudu mizunguko ya mujini…………..”Amen. It was always painfull to me seeing my own daughter in law jumpimg on daladalas, While I could afford her a  vehicle. So yesterday I suprised her with that small gift. She was Amazed!” ? hayo nimaneno yake babamkwe wa ukweli ?? Haya hongera sana wifi yangu, sasa nikiwa Dar utanikomaje na mizunguko ???❤❤❤ you!

Father and daughter moment

Screenshot_2016-01-27-11-27-56-1Ha! Ha! Ha! Nimependaje hii picha! Huyu ni kaka yangu anaitwa Martin Sarungi hapa yupo na binti yake. Nimecheka kwanza kwasababu ya hiyo peace symbol  (✌) aliyo weka mtoto wake. Huyu kaka yangu yeye ni Chadema / UKAWA damu damu. Naona kamridhisha na binti yake? ubarikiwe sana kaka yangu na familia yako yote.

Penny Tenga katika ubora wake

FB_IMG_1453913047946Sister Penny doing what she does best! Kufundisha watu nikipaji cha pekee sana haswa kufundisha watoto wadogo. Sio wote wanaoweza kusoma na kushika pen au chaki wanafaa kuwa walimu / wakufunzi! Ni talanta waliojaliwa nayo watu wachache sanaaaaaa kama huyu dada yangu. FB_IMG_1453914015070Hapa ni siku ya Sabato   (Juma Mosi iliyopita) akiwafundisha watoto maneno ya Biblia kuhusu uumbaji wa Mungu. Penny yeye si mwalimu, ila anahicho kipaji cha kuelekeza / kufundisha watu kwani hata sehemu kubwa ya kazi yake ni kuelekeza watu……Kama nilivyo sema kipaji cha kufundisha watu ni kipaji cha pekee sana, kwakweli mimi sikujaliwa nacho ?? mimi na panick haraka sana na huwa nakuwa confused kama mtu anielewi! Hata mwanangu anajua hilo yupo radhi afundishwe na mtu mwingine lakini siyo mimi ??? nilimfundisha kuendesha gari mbona ilikuwa ni patashika?! Lakini hakuwa na ujanja alielewa tuu mpaka akapata driving license yake. Hakuna ubaya wowote kusema your weakness (es) ni njia moja wapo yakuonyesha kuwa umekomaa kifikra na unajitambua!Hivyo mimi huwa nipo muwazi sana sioni shida kusema my weakness as a normal human being! FB_IMG_1453913081327-1Naomba nimpongeze dada yangu Peninah Tenga kwa kipaji ambacho Mungu amemjalia nacho na anakitumia kama kinavyo stahili, zaidi kwa kumtukuza Mungu. Ubarikiwe sana dada yangu na Mungu awaongoze watoto wetu washikemafundisho yake, Amen!

Manhood

imageMy dad, Mr O.O Igogo,  enjoying himself somewhere in China last week. We thank God for His traveling mercies, he’s safely back home.

Let us support Maryam

Screenshot_2016-01-27-10-34-03-1Nimevutiwa na gukuswa sana na maneno ya #KichunaWaKizaramo hapo juu ☝ ……….Hongera sana Maryam, Mungu akuongoze, akubariki sana,  usiishie hapo tuu bali ukawe the next Christian Amanpour!

Screenshot_2016-01-27-11-29-08-1Wow! Mama akiwa beneti kabisa na binti yake, kwa support na upendo wa mzazi. Hongera sana Linda kwa kuwa mama mwema. Screenshot_2016-01-27-11-31-03-1Wapendwa wasomaji wangu, nawaombeni tum-support mtoto wetu. Maryam pia yeye amejaliwa kipaji cha ushonaji, na amesha onyesha dalili za kwenda mbali zaidi basi tumuunge mkono wapendwa. Yeye anabuni nguo za midoli. Unaweza kuona kazi zake na mambo anayofanya kwa kum-follow kwenye IG yake kwa jina la #Fashionadoz. Mbarikiwe sana mnapo fanya hivyo. Screenshot_2016-01-27-11-28-44-1Once again, Congratulations Maryam and your whole group, wishing you the best of all.

Mother and daughter moment

FB_IMG_1453913754298-1Mama na binti zake. Wamependeza sana.  Mwenye dera la blue hapo kati ni my friend and schoolmate wangu toka Kowak Girls Secondary school iliyopo wilaya ya Rorya, mkowa wa Mara. Yeye anaitwa Maimuna, mwenye dark-blue ni dada yake mkubwa, na mwenye green ni mama yao mzazi. Asanteni sana wapendwa, mbarikiwe mno.

Manhood

FB_IMG_1453913149506-1Binadamu yangu Wakili wa kujitegemea Richard Opiyo  (Katikati) akiwa na marafiki zake ndani ya Ngorongo Crater, Arusha. Mbarikiwe sana

Kutoka Facebook

FB_IMG_1453912859676-1-1Nimependa sana hii picha ya Hawa, from the ‘Queens land’ kapendeza sana na lemba lake. Simple and beautiful!

A word of wisdom

Screenshot_2016-01-22-15-27-09-1FB_IMG_1453913368104-1

The New Yorkers family

FB_IMG_1453657046508I truly love the New Yorkers family, beautiful people with beautiful soul! FB_IMG_1453657035403Guys, you know how to partyy, one day gonna join you ? not like I’m jealous no-no-no! Just want to have fun with ya! ?? FB_IMG_1453657015279Awhh! Look at that msosi, so yummy!FB_IMG_1453657087738Halafu wee mtani  mmh! Unapenda kurusha watu roho kha! And who is that ? yes him!! “Wivu sina lakini roho inauma” ?? Haya bwana, lemme zip it oops! Am typing! FB_IMG_1453657076507Brothers looking shap! ? FB_IMG_1453657023814Siyo siri umetisha mtani wangu! To cute ??

Hot shot of the day

Screenshot_2016-01-24-11-04-51-1Mr and Mrs Mali Kimesera. Naipendaje sasa hii  couple ?? Wamependeza sana. Hapa ni jana wakiwa katika charity event huko Atlanta, Georgia a.k.a “Hotlanta” Georgia.  Safi sana LB na Manager wake mnafanya kazi nzuri mno. Great example to many couples. Mbarikiwe sana.Screenshot_2016-01-24-11-01-32-1Huyu #KichunaWaKizaramo unajua ni level nyingine kabisa! Hiyo nguo aliyovaa Missy LB ni kashona mwenyewe designer wetu waukweli ?  soma hayo maneno aliyo andika basi kama uwamini……… Screenshot_2016-01-24-11-05-24-1Nahivi ndivyo ionekanavyo kwa nyuma. Hongera sana #KichunaWaKizaramo Mungu akujalie ufike mbali zaidi. Pia hongera kwa shemeji yetu kwa kuwa Manager mzuri. Mbarikiwe mno ?

Kutana na Sophia Makoyo

2016-01-21 21.16.32Kwajina naitwa Sophia Daudi Makoyo, naishi Shirati wilaya ya Rorya.  Mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma (UDOM). Nasomea shahada ya kwanza ya sheria  (barchelor of laws). Sababu iliyonisukuma mpaka nikaamu kusomea sheria ni swala zima la haki za wanawake na watoto! Nataka kutetea haki za wanawake pamoja na watoto generally nataka kutetea human rights. Natamania sana siku moja nijiunge na Tanzania Women Lawyers Association (TAWLA) iliniweze kutimiza ndoto zangu. 2016-01-21 21.15.21
 Kuhusu maisha ya chuo; maisha ya chuo yana changamoto especially kwa watoto wa kike hasa pale wanapokosa mkopo wanajikuta wanajihusisha na matendo maovu kama uhuni uliyopitiliza ili waweze kumudu gharama za maisha. Nimtihani mkubwa sana!
Unaelewaje dhana nzima ya mafanikio / success?………Kimtazamo wangu mimi kuhusu mtu kuwa successful; ni hali ya kuwa na mafanikio hasa pale unapofikia malengo yako. Kwamfano mimi naweza sema nipo successfully kwa kiasi fulani kwasababu half of the dreams na goals nilizo kuwa ni me set-up nimefikia. Nili dream kufika form six, kufika chuo kikuuu na kusomea law na nimefanikiwa though sijamaliza B.A yangu but I am almost done! FB_IMG_1453432262183
Katika maisha yangu naumizwa na vitu vingi lakini maisha ya kuwa yatima yanaumiza sana sana hasa pale unapohitaji support ya mzazi wako na unakosa. Unakuwa unajihisi mpweke sana wakati wote, namiss sana mapenzi ya mama yangu, ushauri, na  hasa kudeka deka. Japo nashukuru Mungu sijapata kuona watu waki ni treat vibaya kwasababu ya uyatima wangu. Namimi sijatumia uyatima wangu kama njia yakutenda maovu, au kukwepa adhabu yoyote ile. Siku zote natumia status ya uyatima wangu kwenye maswala ya shule tuu, hasa pale ninapoomba mikopo kutoka bodi ya elimu ya mikopo ya juu HELSB. 
FB_IMG_1453432212379
Unafikiria uyatima inaweza kuwa kikwazo cha mtu kutimiza ndoto zake?………….Mimi naamini kuwa yatima hakutanizuiya kufikia ndoto zangu kwani nakuwa inspired sana na ndugu zangu waliofanikiwa through hard work bila misaada ya wazazi. Japo lazima nikubali changamoto ni nyingi sana, kuu zaidi ni ukosefu wa pesa. Kitu kikubwa kinachonipa furaha moyoni ni kuona kuwa kuna watu nyuma yangu wana nisapoti na wako very proud of me hasa baba yangu Daudi Makoyo kwasababu wanafurahishwa na jitihada zangu. They are very happy to have me. Marehemu mama yangu alinifunza kuwa mtiifu, mvumilivu, mnyenyekevu, na kujifunza kusema neno Samahani / Nisamehe pale ninapokosea. Hivyo naamini hayo mafunzo yake ndiyo yamenifikisha hapa nilipo na naamini yatanifikisha mbali zaidi katika maisha yangu. 
Mwisho, katika maswala ya uhusiano japo siku hizi watu wengi wanaangalia “majina ya familia” lakini sidhani kama kuwa yatima itakuwa kikwazo cha mtu kumpata ukupendaye kwa dhati kwani mtu kuwa yatima si kwakupenda kwake bali ni mipango ya Mungu. Labda cha muhimu niwasihi wasibweteke. Wajitume wajifunze kujitegemea sio kuwa tegemezi kwa wanaume manake success does not come in a silver plate you have to go and get it! FB_IMG_1453432192175

Men in action!

Screenshot_2016-01-23-16-53-50-1Marehemu baba wa taifa na Rais Dr. Magufuli.  Maneno kwa vitendo ????

Some sense of humour

Here’s some stress reliever…………..?

*If swimming is a good exercise to stay FIT, Why are whales FAT ?? ???

*Why is the place in a stadium where people SIT, called a STAND ????

*Why is that everyone wants to go to HEAVEN, but nobody wants to DIE ???

*In our country,We have FREEDOM of SPEECH Then why do we have TELEPHONE BILLS?!???

*If money doesn’t grow on TREES, then why do banks have BRANCHES ? ???

*Why doesn’t GLUE stick to its BOTTLE????

*Why do you still call it a BUILDING, when its already BUILT????

*If its true that we are here to HELP others,What are others HERE for ? ???

*If you aren’t supposed to DRINK and DRIVE…Why do bars have PARKING lots ? ????

*If All The Nations In The World Are In Debt, Where Did All The Money Go? ???

*When Dog Food Is New With Improved Taste, Who Tests It..? ???

*If The “Black Box” Flight Recorder Is Never Damaged During A Plane Crash, Why Isn’t The Whole Airplane Made Out Of That Stuff..? ???

*Who Copyrighted The Copyright Symbol..? ???

*Can You Cry Under Water.? ????

*Why Do People Say “You’ve Been Working Like A Dog”, When Dogs Just Sit Around All Day..?? ???

*Why we Drive on Parkways, and Park on Driveways? ???

*Why do Mosquitoes Suck Blood Instead of Oil so they can gain Weight?! ???

??? Enjoy 07f36d034c256156af62547cfc22ce815f8

Source: unknown

 

Manhood

FB_IMG_1453432126409-1-1Lovely pics of Mr. Madebe. I love the kitinge, very colorful. Be blessed Mr. FB_IMG_1453432126409-1-1-1

Kutoka Facebook

FB_IMG_1453508995439Pendeza sana binti wa mzee Otto! Nimepitiwa na ulivyo vaa na mpangilio wa rangi za mavazi yako ni mzuri sana. Ubarikiwe sana. FB_IMG_1453508963771Simply beautiful!

Blog