Category Archives: politics

“A vindictive askofu……….askofu Gwijima……” Chege Kilahala

Continue reading “A vindictive askofu……….askofu Gwijima……” Chege Kilahala

KATAZO LA KUSAFIRISHA MCHANGA WA DHAHABU -Peter Sarungi

KATAZO LA KUSAFIRISHA MCHANGA WA DHAHABU

Peter Sarungi (The next time)

Sehemu ya I – Utangulizi

Mkuu wa Kaya ali ahidi kusimamia sector ya madini kwa umakini ili sector hiyo iweze kuleta tija na faida kwa Taifa. Hivyo serikali ya Mkuu wa kaya imezuia usafirijashi wa mchanga wa dhahabu kwa makampuni ya uchimbaji yaliyopo nchini kwa muda usio julikana.

Lengo la zuio hilo lililotokana na kauli za mkuu wa kaya ni kuhakikisha serikali ina ondoa mianya ya kuibiwa madini hayo ambayo yana chujwa nje ya nchi huku sisi tukipewa mrejesho ambao kwa hisia za mkuu wa kaya anao mrejesho bado una ukakasi. Lakini pia mkuu wa kaya alitamani kabla ya kuwa Mkuu na anaendelea kutamani kujengwa kwa hilo Tanuru kubwa la kuchuja dhahabu, shaba na copper hapa Tanzania ili kufikia ndoto za kuwa na Tanzania ya Viwanda.

Pamoja na dhamira njema ya mkuu wa kaya, ni vizuri na sisi watanzania tukajua kinachoendelea katika sector hii ili tupate kujua faida na hasara za zuio hili ikiwa ni pamoja na changamoto za kufikia shauku la mkuu wa kaya la kuwa na Tanuru hilo lijulikanalo kama Copper Concetrate Smelter  Hivyo nita toa makala ya kueleza hali halisi za sector hii ikiwa ni sehemu ya kwanza na makala nyingine ya kueleza faida, hasara na changamoto ya kufikia ndoto ya mkuu wa kaya ya kuwa na Tanuru la kuchuja madini hayo Tanzania.

Nitatumia vikao mbalimbali nilivyoweza kuudhuria vya wataalum wa madini, ripoti mbalimbali kutoka TMAA na machapisho mbalimbali ya kimataifa kama vyanzo vya habari katika kusapoti andiko langu.

Asanteni

“Republicans and their “pipe dream” of appealing and replacing Obamacare.” – Chege Kilahala

Republicans and their “pipe dream” of appealing and replacing Obamacare…….

If you can’t marshal enough votes in a house (the congress) where you have a comfortable majority. Then your chance of passing it the senate where you have a very thin majority is non-existent…..

Now, we can toast and celebrate that, Obamacare is the law of the land….and it will carry on being so…….I look forward to seeing a universal healthcare system in the USA; one day soon. Just like whats found in Canada and Scandinavian countries….

UKIMWINDA SANA MJUSI ANAGEUKA NYOKA. -Peter Sarungi

UKIMWINDA SANA MJUSI ANAGEUKA NYOKA. 

Peter Sarungi (The next time)

Huu ni msemo wa wahenga ambao uhalisia wake unaonekana mara chache porini lakini hutokea sana kwa maisha ya binadamu. Naamini kuna watu walisha wahi kumwinda mjusi kipindi walipokuwa watoto na katika kumwinda mjusi gafla walipo toa jiwe wakakutana na nyoka, inapofika hapo lazima hali ya hatari itatokea.

Naiona nchi yangu kwa mbali inakaribisha hali ya hatari. Mkuu wa kaya alianza kuongoza nchi yake kwa misingi ya sheria huku akijitambulisha kuwa yeyeni mkali kwa maneno na matendo yake. Baada ya kuwa mkali sana watoto wakaanza kulalamika huku wakionesha kuto ridhika na maamuzi ya baba. Watoto wakaanza kumwinda baba kwa vifungu vya sheria huku wakimtangaza baba kuwa ni dikteta. Na kwa jinsi baba alivyo na msimamo, hakuwahi kurekebisha makosa yake hasa yale yaliyovunja sheria na hata kuonesha upendeleo wa wazi wazi huku akiwagawa watoto wake kwa kauli na matendo.

Kwa sasa hali imekuwa mbaya maana watoto wameanza kumkana baba yao kwa kutumia mama yao Katiba. Wana mshawishi mama yao (Katiba) awaoneshe baba mwingine kwa kutamka kuwa huyu sio baba mzazi na wamtafute baba mwingine.

Kwa hatua ya mawindo yalipo fikia,  nawaona watoto wanahisi wanaye  mwinda ana fanana na Mjusi hivyo wanaongeza jitiada za makusudi wakiamini nguvu za mjisi zipo mkiani na wala sio nguvu za kuogopesha kiasi cha kutaka kumtoa kwenye pango lake.

Lakini nahofia sana hasira za baba, baba akikasirika na kuamua kutumia nguvu zake basi anaweza akawalazimisha watoto kuendelea kuitwa baba kwa kumtishia mama na hata kuwa adhibu vikali watoto wanao kwenda naye kinyume, na akiona bado anapingwa basi anaweza kumbadili mama mwingine na kufunga ndoa ya kudumu. Kwa hatua hii, baba hatakuwa tena mjusi bali atakuwa ni nyoka.

Kwa sasa watoto wajiandae kukutana na nyoka katika mawindo yao, wasidhani wataendelea kukutana na mjusi walie mzoea kumwinda. Wajiandae na plan B,C na hata C ya kukutana na Nyoka.

By the way baba amesha geuza kichwa bado mkia wa nyoka tu aanze mashambulizi kwa watoto wanao winda. 

“Be careful and watch it” Mkuu wa kaya 24/3/2017

“Did Magufuri’s decision to appoint him as the RC base on the qualification he claimed to have?!!!” -Chege Kilahala

If I apply for a job that requires a qualification A and I get offered the job on the basis of my qualification A, then if my employer finds out that, I didn’t possess that qualification, he/she will have the “legal basis” to terminate my employment on that fact……….But if I apply for a job that does not specify that it requires any qualification, but I falsely put down that I possess qualification A, my employer WOULD NOT HAVE any legal basis to terminate my employment on that fact. It is because, his decision to employ me was not influenced by the fact that I have  or have not had that particular qualification.

For that reason, why do people ask for the resignation of Paul Makonda from the RC position? Did Magufuri’s decision to appoint him as the RC base on the qualification he claimed to have?!!! Do you need to even have a standard 7 qualification to be appointed as an RC??!! Leave the guy alone………….!!!

“Sikiliza Zitto Kabwe” Jerry C. Muro

Sikiliza Zitto Kabwe

Mungu amewapa wenzetu “wazungu” baraka ya utajiri wa technology.

Na pia ametupa sisi watanzania baraka ya utajiri wa Udongo wenye thamani.

Ili technology yao ifanye kazi inahitaji malighafi kutoka kwetu.

Sio busara na hekima kuwapelekea malighafi wao mana haiwezi kuhamishwa, ILA TECHNOLOGY INAHAMISHWA.

WAJE WALETE TECHNOLOGY TUTAZUNGUMZA NAO. Jerry C. Muro

Machame, Hai

Kilimanjaro.

26/03/2017

KAMA NAPE KAFANYIWA HAYA, VIPI KWA MTI MKAVU?. -Peter Sarungi

Peter Sarungi (The next time) Injili ya yesu ilipata kumnukuu Nabii Issa (Yesu Kristu) alipokuwa njiani kusulubiwa baada ya kukutana na wamama wakimlilia kwa uchungu,  sehemu ya nukuu inasema ” ikiwa wanafanya haya kwa mti mbichi, je itakuwaje kwa mti mkavu???? 

Kwa kawaida mti mbichi una sifa za kuvumilia shida, ni mgumu kuvunjika lakini vilevile ni mti unao onesha uhai, wenye kuwa na afya ya kustawi na ni mti unao weza kuzaa matunda tofauti na sifa za mti mkavu ambao kwa ujumla unatambulika kama mti ulio kufa.

Namfananisha Mh. Nape Nnauye na mti mbichi ndani ya CCM. Kila mtu anajua mti huu mbichi ulivyo kuwa na uhai, wenye afya na aliyeweza kuitetea chama hadi kupata matunda ya kushika hatamu. Nape amesema alilala porini siku 28 kwaajili ya kuhakikisha chama inapata ushindi, amekipigania chama hadi kufikia kutoa utu wake kwa kukubali lawa, dhiaka na chuki kutokana vita ya kutetea chama kipindi kigumu cha uchaguzi 2015. Inawezekana ile kauli ya Bao la Mkono aliyosema Nape ndio aliyokuwa akitumikia porini kwa siku 28.

Lakini leo, Mti huu hauna tena dhamani mbele ya bashite, mti unatendewa yale wanao tendewa wapinzani wa leo. 

Ikiwa haya yametendwa kwa mti mbichi kama Nape, Je ni nani aliye salama hasa kutoka mti mkavu kama mimi?????

Pole Nape, najua sasa zile akili za kushikiwa na chama utakuwa ume waachia wengine ambao bado wana imani ya kuchukua nafasi yako.

By the way wewe unaye jiita mwana CCM na mkereketwa wa zidumu fikra za mwenyekiti, anza kujiandaa kisaikolojia ili usije pata strock kwa maamuzi kama haya. Chama kwa sasa kina mwenyewe….

Baba yangu Dr. Magufuli mbona unatuangusha hivyo?!!- Alpha Igogo

Baba naomba nianze kwa salamu; shikamoo baba!…….Baba naomba nikwambie dhumuni la barua hii si kukuomba hela za matumizi kwani hilo si tatizo langu kwa sasa! Pesa zipo tena wewe wenyewe ndio umeziweka hivyo nipo vizuri baba!

Alpha Igogo, Blogger

Baba ninachotaka kukwambia leo hii nakuomba utege masikio yako kwa makini sana baba yangu kwani mwanao nimejawa na hofu nyini sana! Wewe ni baba yangu ninaye kupenda sana na siku zote nilitembea bara-barani na kulala usingizi mnono sana nikijua tupo katika mikono salama! Lakini, sasa hivi uwoga umenishika sana, siyo tu kwa watu ambao siwajui bali hata kwa hawa wakuu wa mikoa yetu ulio wachagua. Na mbaya zaidi imani yangu juu yako imeshuka kwa kiasi kikubwa sana kitu ambacho si kizuri kabisa kwani wewe ni baba yangu!

Baba, naomba unisaidie kuelewa, kwani unampango wa kung’ang’ania madarakani? Au unataka nchi yetu iwe kama Rwanda ile ya mauwaji?  Au kama Uganda ya Mseven? Au unatamani Tanzania iwe kama Congo ya Kabila, na Burundi ya Nkurunzinza?! Au iwe nchi ya ukabila kama ile nchi ya Jomo Kenyatta?!! Mimi sijui baba lakini natamani kujua, tafadhali nijuze ili nijuwe kama nianze kuomba ukimbizi nchi za jirani?! Nakama ni hivyo je, zitakua ni nchi zipi katika bara hili la Africa?!!

Baba, niwapi mimi binti yako nikimbilie maana dalili zinaonyesha kama hali itaendelea kuwa hivi na wewe ukaendelea kubariki kwa mikono yako miwili basi mimi mwanao sina budi kuanza kukimbia kuomba hifadhi nchi za jirani hata ng’ambo ya Magharibi kama itaibidi! Japo natafakari sana je nitakimbia mwenyewe au nimchukuwe na mama? Vipi kuhusu bibi na babu? Bila kumsahau mjukuu wako kipenzi! ooh! vipi na yule dada yako wa pekee aliye olewa kijiji cha Koromije mkoani Mwanza? tena yeye ni mlemavu wa miguu! Na binamu yako Zainabu ambaye ni mlemavu wa ngozi huwa awezi tembea juani! Hawa wote nawapenda sana na itakuwa ngumu sana kwangu mimi kuishi mbali nao, nifanyeje baba? Hivi mida ipi itakuwa mizuri kwetu sisi kuanza mwendo; mchana au usiku? Baba, nguvu zinaniishia! Baba kwani niwapi tulikosea? Mbona mambo yanakuwa tofauti na ahadi zako? Mimi niliwashawishi ndugu zetu wote, majirani, marafiki, na Watanzania wote kwa ujumla kuwa wakupigie kura ya “ndio” kwani nina imani nawe, na kwa uchapa kazi wako ulionyesha kuwa wewe unafaa sana! Nao kwa furaha na nderemo wakakupitisha kwa kishindo kuwa Rais wa nchi yao. Nami mwanao nikatembea kifua mbele tena kwa mikogo na madaha mengi sana kuwa sasa Tanzania mpya inakuja! Tanzania ya amani tele, iliyo jaa demokrasia nyingi na uhuru wa kujieleza bila vitisho! Tanzania ya viwanda na miundo mbinu ya kisasa!

Baba, sasa mbona mambo yanakwenda sivyo?! Uliahidi kuleta uongozi bora ulio tukuka, uongozi wa haki na wakufuata sheria. Uliahidi kutulinda sisi wanawake na watoto, ukatuhakikishia kuidumisha amani ndani ya nchi yetu tuipendayo sana! Imekuaje sasa? mbona wavunja sheria ndio unawatukuza na kuwatunuku shahada za uongozi bora?! Baba ni wapi tumekukwaza? Mbona viongozi wanao tishia usalama wa maisha yetu kwa kuvamia sehemu zetu za kazi kwa mitutu ya bunduki ndio unao wapenda sana? Usalama wetu upo wapi? Mbona ndugu zangu hata hawaruhusiwi kuongea kwa uhuru bila kutolewa silaha za moto?!

Baba, nampenda sana kaka yangu ambaye ulimchagua kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam. Nimchapa kazi sana hilo halina upinzani lakini baba yeye si mkamilifu, ana mapungufu yake kama mwanadamu yoyote yule; hivyo kubali kuwa sanyingine naye hukosea. Basi anastahili kuadhibiwa kama unavyo tuadhibu sisi wanao wengine kwa makosa tunayo yafanya au pale tunapo kukwaza!

Baba, sababu ya mimi na Watanzania wengine kuomba umuadhibu huyu kaka yetu, si mbaya hata kidogo! Hatuna nia ya kumkomoa au kumuumiza bali nikutaka kuweka mfano mzuri kwa wadogo zetu ambao wanakutizama iliwajifunze kitu fulani kuhusu utawala bora wa sheria na haki. Maamuzi yako  yatatuaminisha kuwa unamaanisha kile usemacho. Kufanya hivyo kutaondoa hofu tulionayo Watanzania. Au unaogoapa hutopata mchapa kazi kama yeye? mbona kule kanda ya ziwa wapo wachapakazi wengi sana, tena watiifu, na waaminifu, hawana uonevu wala kiburi?!

Baba, naomba nimalizie kwa kusema samahani sana kama tumekukosea. Lakini ukumbuke tu kuwa wewe ni baba wa wengi na si wa mtu mmoja tu, hivyo tunaomba utupende, na utulinde wote bila ubaguzi wa aina yoyote! Usitugawe baba sisi sote ni wana wako. Sisi ni ndugu moja japo wengine ni wembamba na wengine wanene. Japo wengine wafupi na wengine warefu, wengine weusi wa rangi ya ngozi na wengi ni maji ya kunde; sisi ni ndugu moja. Usitubague wala kututenga!

Asante sana baba.

KUNA GHARAMA KUTETEA UKWELI – NAPE!

KUNA GHARAMA KUTETEA UKWELI – NAPE

Peter Sarungi (The next time)

Nimesikitishwa sana na taarifa kutoka ikulu, ingawa niliona ishara hiyo kutokana na mwenendo uliopo. Pamoja na hayo Nampongeza sana Mh. Nape Nnauye kwa karata ya ushindi aliyo cheza jana kwa maamuzi ya kutetea ukweli. Kwa karati hii, watanzania wamefuta Hasira, dhiaka na chuki walizokuwa nazo toka kipindi ulipo kuwa Msemaji wa propaganda za chama. Leo Umekuwa shujaa wa uhuru wa habari na naamini hivi vyombo vya habari vitakutunuku kwa maneno na matendo kwa kutetea ukweli. Nakutakia safari njema ya siasa, ukiweza basi anzisheni chama chenu wanasiasa wote mnao tengwa na chama kwa kuwa tofauti na mkuu maana sioni chama mbadala kitakocho wapa uhuru wa kufanya siasa zenu.

“TLS ; CHADEMA’s legal department or another opposition party?!!!” – Chege Kilahala

TLS ; CHADEMA’s legal department or another opposition party?!!! There are legal boundaries within which these institutions can carry out their daily duties……using TLS as a mouthpiece to pursue some political agenda is a no-no-no-no!!!  

UKIPINGWA NA MKUU, VIZURI UKAJIWAJIBISHA. -Peter Sarungi

UKIPINGWA NA MKUU, VIZURI UKAJIWAJIBISHA!

Peter Sarungi (The next Speaker)

Ingawa ni vigumu kupata tamaduni za kuwajibika kwa viongozi wengi wa Afrika lakini bado kuna kila ulazima wa kuwakumbusha viongozi wetu na hata kuwafunza vijana ambao ni kizazi kinachochukua dhamana kutoka kwa wazee wetu juu ya umuhimu na faida za kuwajibika mwenyewe bila kushurutishwa.

Watanzania tunafunzwa na viongozi wetu kuwa na tabia za ajabu sana unapopata madaraka, tabia kama za ubabe, majivuno, dharau, ung’ang’anizi, ufisadi, uzembe na zingine nyingi ambazo tumekuwa tukizishuhudia kutoka kwa viongozi wetu. Tamko alilotoa Waziri wa Sheria la kupiga STOP ufungaji wa ndoa bila cheti cha kuzaliwa kuanzia mwezi wa tano na baada ya muda mfupi Mkuu wa kaya akatoa katazo la utekelezaji wa agilo la waziri wake. 

Kwa tafakuri ndogo, inaonesha kwamba agizo hilo la waziri halikupata utafiti wa kutosha na pia halukupita kwenye vyombo vya ushauri kama Baraza la mawaziri. Pia inaonekana agizo hilo limemkera sana Mkuu wa kaya kiasi kwamba akalitolea tamko yeye mwenyewe bila kutumia wasaidizi wake kama vile waziri aliye husika kutoa agizo hilo.

Kwa maamuzi aliyoyafanya Mkuu wa nchi kwa Waziri husika lina fundisho kubwa sana na angalizo kwa waziri husika. Ningekuwa mimi ni waziri husika ninge jiwajibisha kwa kushindwa kufikia viwango vya mkuu wangu wa kazi, maana inawezekana akanitumbua ama akanisahau kwenye marekebisho ya baraza la mawaziri.

Nafikiri ni muda mzuri kwa Waziri Mwakiyembe kuji pumzisha ikiwa ni hatua ya kujiwajibisha ili aendelee kubaki na heshima yake iliyo tukuka kwa nchi. Kuna faida kubwa ya kujiwajibisha mwenyewe kuliko kusubiri kuwajibishwa tena kwa aibu, nasema hayo kwa sababu na mimi mpaka leo naendelea kunufaika na hii tabia ya kujiwajibisha ambayo nimewahi kuifanya sehemu mbalimbali za uongozi wangu.

By the way kuna kazi sana kutoa tonge kutoka kwenye midomo ya waafrika, wapo tayari kunyang’anywa kwa nguvu kuliko kulitema wenyewe hata kama tonge ni chungu.

Asanteni.

“NIMECHAGUA UKWELI KWENYE SIASA, SIO BARIDI WALA MOTO.” -Peter Sarungi

Peter Sarungi (The next Speaker)

Siasa safi zinahitaji kuwa na demokrasia ndani yake, kuwe na uhuru wa kutoa mawazo mbadala, kuwe na desturi ya kuvumiliana hasa pale mnapopingana mawazo na kuwe na tabia ya kutafuta na kusema ukweli hata kama ukweli huo utakuwa mchungu.

Mtindo wa vijana wengi wa sasa ni wa ajabu sana katika siasa. Mtindo ulio gubikwa na tabia za uongo, unafiki, fitina, wasaliti, ndumilakuwili, kujipendekeza, kutafuta sifa, kukurupuka, ushabiki, na unazi usiokuwa na tija kwa taifa. Tabia kama hizi zina fifisha ubunifu, uzalendo, umakini, ujasiri na umahiri kwa vijana katika uongozi na uwajibikaji.  Tumejenga jamii ya vijana walio gawanyika kihisia, itikadi, maneno na kwa matendo yao, waoga wa kutetea ukweli, wepesi wa kushindwa na uovu, walio tayari kusema vya kukaririshwa. Ndio maana kuna vijana walio tayari kukosoa jambo lolote kutoka upande wa pili hata kama ni jambo jema kwa taifa na wapo tayari kusifia jambo lolote la upande wao hata kama ni sumu kwa Taifa. Wameamua kuwa baridi ama moto.

Mimi nimekataa kuwa sehemu yao, kuwa mtumwa wa fikra zao, kutumika katika malengo yao. Nimeamua kuwa mfuasi wa ukweli na kwa fikra huru. Nahitaji Ukweli ili uniweke Huru, ukweli utakao tibu Taifa ili vizazi vijavyo vipate kufaidika na ukweli huu.

Unga kuchagua ukweli ili tujenge Taifa lenye kuheshimu ukweli.

Asanteni sana.

KIIZA TUNDU LISU BASIGYE KOROKONI- Peter Sarungi

Peter Sarungi (The next Speaker)Ipo siku masikio yata ona badala ya kusikia na macho yatasikia badala ya kuona. Wakati ambapo utatamani ujifiche chini ya milima lakini haitawezekana, wakati ambao wanawake wengi wataomba kuitwa kwa jina la mwanaume mmoja huku wakijilisha na kujivisha wenyewe.

Kwa sasa namfananisha Tundu Lisu na mwanasiasa mkongwe wa vikwazo kutoka kwa jirani zetu Uganda Mh. Kiiza Besigye. Kwa hivi vikwazo vya kuwekwa korokoroni na kupewa kesi nyingi za uchochezi kwa Mh. Tundu Lissu huku akiendelea kuwa jarisi na mwenye kutetea ukweli na hata kutenda na kuheshimu sheria. Sasa ninaona umuhimi wa Tundu Lisu kuwa Raisi wa TLS maana kwa sasa tunahitaji viongozi wanao hoji mifumo kandamizi bila uoga ili kulinda maslahi ya Taifa na watu wake. Kwa courage aliyonayo Mh. Tundu Lissu katika siasa za kweli, naamini hichi ni kipindi cha watu kama akina Lissu kunyanyuka na kuungwa mkono kwa makusudi.

Ningekuwa ni mwanasheria, ningemchagua Lissu kuwa Raisi wa TLS. By the way hiyo TLS na majukumu yake nimeifahamu kipindi hiki kupitia Lissu na inawezekana sio mimi tu, tupo wengi.

Asante Lissu, Go go go go Lissu

TAFAKURI YA LEO JUU YA WABUNGE WA CCM.- Peter Sarungi

Peter Sarungi (The next Speaker)

Tabia ya wana siasa kabla ya kuwa watawala ni kama tabia za wachumba ambao bado hawajafunga ndoa. Tabia yao kuu ni kuhaidiana mazuri, kusifiana, kuelekezana kwa lugha ya kuvutia, kutiana moyo, kuoneshaana upendo wa agape lakini pia kuna tabia moja mbaya ya walioyo nayo ya kuficha udhaifu wao na mabaya yao.

Kila inapoitwa leo, napata fursa ya kujua tabia za mkuu wa nchi kupitia kauli zake na matendo yake. Niliwahi kukiri hapo mwanzo kwa kusema kuwa Mkuu wa kaya anasimamia vizuri kauli na matendo yake wakati wa kampeni nikidhani ataendelea kutawala kupitia kauli zake za kusisitiza umoja wa nchi. Nahisi ni mihemuko ya muda iliyo niathiri.

Pamoja na changamoto hizo bado maisha na siasa zitaendelea na ni lazima tuendelee kuwaoma wabunge hasa wa CCM ambao ni 75% kusimamia kwa kuikosoa, kuisema na hata kuipongeza serikali wanapo kuwa bungeni maana hiyo ndiyo kazi tuliyo watuma. Pamoja na mtikisiko huu ulio wapata wabunge kutoka kwa Mkuu wa kaya kama ilivyo ripotiwa na gazeti la mwananchi bado mtaendelea kuwa wabunge mlio pewa dhamana na wananchi ya kuwa wakilisha bungeni katika kuisimamia serikali.

Tusijenge Taifa la chuki na uadui unao tokana na siasa, tuki ruhusu hilo basi hatutokuwa salama maana ukweli ni kwamba chuki na uadui havina mipaka, nikikuchukia kwenye siasa usidhani nitakupenda uraiani. Hiyo ni mbegu mbaya itakayo tafuna jamii yetu.

Tujitahidi kujenga jamii ya kuvumiliana, kushauriana, inayo heshimu fikra tofauti na inayoweza kuwa karibu hata kama watakubali kutokukubaliana.

Mungu tubariki huko tuendako.

TAFAKURI YA LEO JUU YA CCM MPYA -Peter Sarungi

Peter Sarungi (The next Speaker)

Nimepata taarifa juu ya kuzaliwa CCM mpya iliyo badilika katika muundo wa chama na uendeshaji lakini ikiendelea kubaki na itikadi yake ya zamani. CCM Mpya iliyosemwa na mwenyekiti wake kwamba itakuwa chama kwa wanachama yaani chama kitakacho milikiwa na wanachama wenyewe tofauti na mwanzo. Inasemekana kabla ya upya huu, chama kilikuwa kina endeshwa na wanachama wenye nguvu za fedha, vyeo na hata umaarufu. Sasa kwa upya huu, chama kitaendeshwa hata na mlalahoi bila kujali umaarufu wake, cheo chake ama fedha zake… (SAFIII SANAAA..) 

LAKINI..????? Tafakuri yangu ni jinsi gani chama hiki kitaendeshwa na kumilikiwa na wanachama kama inavyoitwa CCM Mpya… ………Ikiwa kiwango cha uwakilishi wa wanachama hawa kwa idadi katika vikao muhimu na vinavyo toa maamuzi muhimu ya chama umepunguzwa kwa zaidi ya nusu??? Yaani kutoka mia tatu na kitu hadi mia moja na kitu..!!!Ikiwa idadi ya vikao vilivyokuwa viki tathmini utendaji wa chama na serikali vimepunguzwa???Chama chenye wanachama na wapenzi wapatao milion 8, kutoka mikoa 35, ikiwa na jumuiya mbalimbali karibia tano na matawi lukuki, chama kinacho ongoza nchi kuongozwa na wajumbe 165 badala ya 385 alafu tuna sema CCM mpya ya kumilikiwa na wanachama??

Hili panga ni kali na sijui kama hawa vijana wenzangu Benard R. Shigela ?na Yesaya Shamsele ?walio anza vizuri kujifunza siasa na uongozi kama watapata nafasi na fursa ya kuwepo kwenye vikao vya CCM mpyaJJk alidokeza sababu ya mabadiliko haya kuwa ni UKATA…. Tunasoma Namba.. Hii sababu ya kuifanya CCM kumilikiwa na wanachama bado kwangu haija ingia akilini labda wadau watufafanulie..

Dr. Magufuri and the agricultural policy…….?!!! -Chege Kalahala

Is he a firm proponent of a free market economy or he simply “dont get it” with regard to the economics behind the agricultural industry???

Or are we witnessing the absence of “coherent and consistent” agricultural policy?

Magufuri told farmers that, the govt will not provide assistance in case of food shortage…..the implication is that, it will be farmers’ fault that there will be food shortage…….mhhh!!

Overall, this just says one thing; either there is no such a thing as an agricultural policy or it is not well developed to reflect some unforessen contingents like bad weather.

European have Common Agricultural Policy(CAP); that have emerged from its birth in the 60s. The aim is simply this; to help farmers in case there is a need for that. The philosophy behind the policy is that, unprotecting the industry will lead to food shortage. What else? Prices fluctuations caused by alternating good and bad season is not a welcome for a smooth economic growth of any country. To stabilize agricultural products prices, and ensure a good standard of living for its citizens, countries enact these kind of policies. 

USA has what it calls Agricultural Adjustments Act; with the same goal. The policy has evolved from its inception in the 1930s.

Tanzania should not second-guess itself when it comes to the agricultural sector. The industry needs govt protection. Magufuri’s statements were so unfortunate.

If more diverse economies; less-dependent on agriculture as the engine of their economic growth like EU and USA have the policy in place,…..why not Tanzania?!!!

CCM WANA HAKI YA KUFUKUZA WASALITI. -Peter Sarungi

Peter Sarungi (The next Speaker)

Huwa sipendi kuingilia siasa za ndani za vyama  vingine lakini huwa inanilazimu kwa sababu chama kama cha ccm kinatawala serikali hivyo maamuzi yake yana athari kwa uendeshaji wa serikali na Taifa kwa ujumla.

Nimeona mjadala wa wafuasi wengi wa upinzani wakilalamika juu ya maamuzi ya fukuza fukuza ya wanachama wa ccm wanao itwa wasaliti. Wanapinga na kulaani maamuzi halali yaliyotewa kutokana na vikao halali.

Mimi naunga mkono maamuzi hayo maana watu walio fukuzwa wamepatwa na mazingira ya kusaliti chama. Ni kama Mh. Zitto alivyo vuliwa uana chama wa Chadema Tanzania kwa tuhuma za usaliti ulio elezewa na viongozi wa kushirikiana na chama tawala. Walio fukuzwa wana mazingira ya kusaport harakati za Lowasa Edward kushika dola kupitia vyama vya upinzani wakati wao wakiwa na vyeo katika chama cha ccm, huu ni usaliti usio takiwa kufumbiwa macho. 

Fukuza, fukuza, fukuza hadi wale wote karibia 75% ya wajumbe wa almashauri kuu ya NEC walio imba wimbo wa kuwa na imani na Lowasa wafutike katika vyeo vyao ndani ya ccm, mkìweza wafukuzeni na wabunge ambao bado ni waumini wa Lowasa.

Mkiamua kujenga safu ya mwenyekiti wenu kwa mgongo wa kusafisha chama, nawashauri mfanye kwa uhakika na asibaki hata mmoja aneyeweza kuhoji na hata kusema tofauti na mkuu. Hilo ni jambo lenu la ndani na wala sisi tusio wanachama hatupaswi kuingilia na ndio maana nina pinga kwa nguvu zote wanao laani na kubeza maamuzi haya.

Nawatakia mkutano mwema katika kujenga ccm mpya na kuiacha ccm ya Nyerere, ccm ya mwinyi, ccm ya mkapa na hata ccm ya Jk.

Poor Makonda…! by Chege Kalahala

Chege Kilahala

In politics, don’t ever let your opponents have a chance “to define” you before you have defined yourself. Thats why politicians in the western world like to write books about their life stories. It gives them a chance to “set the records straight” before their political opponents hijack their stories and paint them however they see fit.

Considering his background, Makonda should have dealt with his past a while ago……! And he still can……..

Mh. Paul Makonda

He has a personal story to tell….of a guy who…despite many obstacles….swam against the tide to reach where he is…..a story that can resonate with a lot of aspiring young men and women…..from all those failures in school and yet be able to pick up yourself and get going…..thats inspiring….! Of course, he will have to start by admitting his blunder and failure to be honest with Tanzanians upfront……My wish is that, there were good PR (public relations) experts in Tanzania….

Well….what can we do?!

“SI KWAMBA NI MCHAPA KAZI TU BALI PIA NI MZURI WA MUONEKANO” Mkuu wa kaya

Peter Sarungi (The next Speaker)

 Moja ya sifa ya Mkuu wa kaya katika hotuba zake ni kupenda kutoa mifano ama utani yenye chembechembe za ukweli. Sifa kama hizi akipewa mama, mke, dada au hata bibi inaleta furaha na inajenga kujiamini kwao.

Nitumie fursa hii kumpongeza Mama Salma Kikwete (Malkia wa nguvu wa Taifa) kwa kuteuliwa kuwa mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Naamini sifa ulizo pewa na Mkuu zita akisi uwezo wako wa kutetea maslahi ya Taifa na wananchi wake.

Nafasi uliyopata sasa inakusogeza karibu zaidi na matatizo ya wana wa nchi lakini pia inakupa uwezo zaidi ya kuleta suluhisho ya matatizo hayo tofauti na ulivyokuwa First Lady. First Lady ni ceremonie title, ulikuwepo kwaajili ya kupamba kazi ya baba, kumshauri na kusapoti kazi zake kupitia WAMA. Uwezo wako binafsi ulifichwa ndani ya mafanikio na sifa za baba. Sasa ni zamu yako kuonesha ushujaa wako kwa nchi na hasa kwa wale wanao beza uteuzi huu, onyesha umuhimu wa fursa kwa wamama kama alivyo onesha Mama Hilary Clinton.

Nakutakia Kazi njema na utendaji mzuri katika kutumikia wananchi wa tanzania kupitia Bunge. Mama usiogope kukemea na kusema ukweli. Ni Haki yako kusema ukweli hata kama utabaki peke yako, bado ukweli huo ulio usema utaishi zaidi yako.

Asanteni.

HIZI KESI ZINA DHOOFISHA SANA UPINZANI- Peter Sarungi

Kuna msemo unasema “Adui mwombee njaa, atainua mikono juu hata kama ni Shujaa”

Msemo huu unatukumbusha kwamba siku zote binadamu umuombea mabaya mpinzani wake, ndivyo tulivyo umbwa na hata katika siasa ndivyo ilivyo tena ni zaidi ya kuomba mabaya na kutenda mabaya kwa mpinzani wake.

Upinzani una kabiliwa na kesi nyingi sana katika mahakama zetu. Kesi hizi zipo kwa viongozi kuanzia ngazi ya ya mwenyekiti Taifa hadi kwa wenyeviti wa vijiji mikoani. Uwepo wa kesi hizi zina athiri upinzani kwa njia tatu.

1. Ki Uchumi: Uendeshaji wa kesi una gharama kubwa mno na kwa nchi zilizoendelea, kesi ni njia moja wapo ya kufilisi au kupunguza uchumi wa mtu ama kampuni. Mfano: Mike Tyson pamoja na mambo mengine ali filisika baada ya kugharamia kesi yake ya kubaka.

2. Ki Siasa: Baada ya uendeshaji wa kesi, kinacho fuata ni hukumu. Hukumu yaweza kuwa nzuri ama mbaya kwa upinzani, inapokuwa mbaya inaleta pengo kubwa la kisiasa kwa upinzani. Mfano: Mh. Peter Lijualikali (MB Kilombero) anatumikia hukumu ya kifungo cha miezi sita jela. Hukumu hii ina dhoofisha nguvu ya siasa na hata kuleta pengo la utendaji wa mwanasiasa huyu kwa walio mchagua.

3. Ki Jamii: Inapotokea kiongozi wa kisiasa anapatwa na tuhuma, anashitakiwa na kuhukumiwa basi wanao umia kisaikolojia ni jamii yenye imani kubwa na kiongozi huyo. Mfamo Mh. Mbowe (MB Hai, KUB na M/kiti Chadema) anapopatwa na tuhuma ya kukwepa kulipa kodi au kujihusisha na Dawa, wanao umia zaidi kisaikolojia ni wakereketwa, wapenzi, mashabiki, wananachama na viongozi wa Upinzani walio chini yake.

Hizo njia tatu kwa pamoja zinaleta athari za kudhoofika kwa wanasiasa mahiri na machachari wa upinzani

#Kumbuka Dhamani sio ushindi, Tunaye kaimu judge mkuu kwa mhimili huu, Kuna wanasiasa walio nyamaza baada ya kesi. Pole G. Lema (MB Arusha) na wananchi wa Arusha kwa mateso ya kisaikolojia mliyo yapata kwa muda wote.