Category Archives: General education

Siku ya maisha yangu: Ndani ya maisha ya designer Kiki Zimba

 “Siku ya Maisha Yangu na @kikizimba @kikisfashion Siku Ya Maisha Yangu Ni show inayo onyesha maisha ya kila siku ya watu mbali mbali wanao toka kwenye mazingira tofauti. Tuna angalia wafanya biashara, wajasiriamali, wana siasa, watu mbali mbali Walio fanikiwa kwenye kazi zao mbali mbali, wakurugenzi, washawishaji, watu wanao julikana kwenye jamii, Na watu ambao wanafanya vitu vikubwa kwenye jamii hata Kama hawa julikani. Je kwenye Siku Yao huwa wana fanya nini tangia Asubuhi mpaka wana maliza siku? Je nini kiini cha mafanikio Yao Na vitu gani vina wasukuma kufanya mambo mengi makubwa wanayo yafanya. Lengo la kipindi cha Siku ya Maisha Yangu Ni kujifunza, kuhamasisha, kuwezesha, kushawishi kupitia watu mbali mbali. Nenda kwenye Bio Na fungua link kuangalia kipindi. #sikuyamaishayangu #kikizimba #kikisfashion” Dorothy Kipeja

LeMutuz: DANUBE sio Chama cha Siasa au anything ni Kampuni ya Biashara ambayo inatoa ajira kwa Vijana wa Kitanzania kama 3,000 na inalipa kodi

LIVE HARD TALK:- The Art Of Business decisions ni maamuzi magumu ya Kibiashara ambayo huwa hayajali local au international Politics huwa ni maamuzi MAGUMU ya kibiashara yanayojali PROFIT kwanza sio Siasa wala anything nilitaka tu kumsaidia aliyeandika hii habari na habari zote zinazotrend kuhusiana na hii ishu ya uamuzi wa Kibiashara ….DANUBE sio Chama cha Siasa au anything ni Kampuni ya Biashara ambayo inatoa ajira kwa Vijana wa Kitanzania kama 3,000 na inalipa kodi kama inavyotakiwa kwa mujibu wa Sheria ila Tanzania hatuna sheria ya kuyaamulia Makampuni ya Biashara nani wa kuwatangazia matangazo yako ya Biashara …ndio maana hatujawaamulia Yanga kusajili Wachezaji wa Bongo tu na hatujawaamulia Simba kusajili wachezaji wetu tu wa Bongo ….kama Dunia ingekuwa na mawazo mgando kama huyo muandishi juu ina maana Samatta asingeweza kwenda kucheza Ulaya kwani kule Belgium hakuna wachezaji? …guys kabla hamjaandika mawazo yenu finyu muwe mnafikiria kwa upana kuwa hizi Social Media zinasomwa Dunia nzima na hasa huko Nje ya nchi sasa wakisoma mawazo madogo kama haya watatushangaa sana kwamba eti kuna wananchi Tanzania hawajui maana ya Global Community & Outreach …DANUBE wameamua maamuzi ya kibiashara na wanazo Justifications as a FACT kwamba @zarithebosslady & @diamondplatnumz ndio Celebrities maarufu sana Tanzania sasa hivi na hata East Africa nzima wao wawili Combined wana wafuasi 7M humu Instagram HAKUNA WENGINE….sasa ungekuwa wewe unamiliki hiyo biashara unasema utampa yule Miss Tanzania asiyejitambua anayegombana mpaka na Kamati ya Miss Tanzania wenyewe na ana Wafuasi wasiozidi 500 tu ndio awe Balozi wako wa Biashara kama DANUBE BIG BRAND? au Super Couple with 7 Million Followers? hahahaha ….I mean kuna mambo yanachosha sana humu Instagram sometimes ila tutaendelea kuwaelimisha tu kwamba haya mambo ya mateam yenu Uchwara msiyaingize kwenye biashara za watu cause Yanga na Simba hawajavunja Sheria kuwasajili Tshishimbi na Okwi so hata DANUBE hwajakosea kumpa deal Zari ni maamuzi ya Business…I hope nimewasaidia wengi at large! …na this topic is CLOSED! – le Mutuz

 Tatizo la watu wenye makelele na muda wa kuandika ujinga kama huyo kaka / dada ni watu ambao biashara yao kubwa kukaa kwenye social media kutukana watu na kueneza chuki! Hamna wanachokijua zaidi ya matusi! Inasikitisha sana hii generation itakayokuja kutawala taifa letu kwani wengi wao akili zao ni za “kupewa”! Hamna kitu wanaweza fikiria kwa akili yao wenyewe ili kutofautisha Tui la Nazi na maziwa!! So sad!………..You go Zari!!

“MUDA huongea sana…..Muda hutenganisha ukweli na Uongo” ~~~~ Dina Marios

MUDA huongea sana.....
muda huponya..
muda hutibu majeraha...
Muda hutenganisha ukweli na Uongo....
Muda Hutoa majibu
Muda hukomaza n.k

Katika jambo lolote lile lipe muda 
Hata ukishika mimba si unaipa muda ili ikue na mtoto azaliwe?
Hata ukipanda mbegu shambani si unazipa muda zichipue na baadae mazao yakue na kuja kuvunwa.
Hakuna jambo linakwenda kwenda tu yoote yanakwenda na muda. Basi hata maswali ujiulizayo ambayo hujapata majibu,yape muda ipo siku utapata majibu.

Kuna mambo huko nyuma nilikuwa sina ujuzi nayo....sina taarifa nayo lakini baada ya MUDA nikayajua na kujifunza.

Hivi unajua uliwahi kuwa mtoto mchanga?unaelishwa na kunyonya?unavalishwa nepi ya vipande vya khanga lakini MUDA ulipita sasa upo hivyo ulivyo.
Katika kila jambo lipe muda.....good morning

Je, Zari ataweza kubeba “bendera” za nchi mbili!?!

  Katika Biblia kuna maneno yanasema ‘hakuna mtu awezae kutumikia mabwana wawili’! Yani kiufupi lazima mmoja utampendelea na mwingine utamuonea kwa mapenzi ya uwongo! Sasa, wote tumeshuhudia maisha ya Zari na Ivan mpaka kuachana kwao. Lakini pamoja na hayo Ivan bado hakuona mtu mwingine ambaye angefaa kulinda mali zake, watoto wake, na kuhakikisha kuwa his Legacy forever lives zaidi ya Zari. Na Zari mwenyewe kwa mdomo wake alitamka mbele ya kadamnasi siku ya mazishi ya Ivan Ssemwanga  (SomaHapa) kua atavaa viatu vya Ivan Ssemwanga, kwani yupo tayari, anaona kama she was prepared enough for it!!  Na kwamba she will do it for his boys, his family, friends, and his legacy!  Swali ambalo ninajiuliza will Zari be able to be a “flag bearer” for the two men from different countries?!  Can she honestly, sincerely, and lovingly serve the “two masters”! ……..Personally, I’m not sure but very curious to see how will this go down considering one of her “men” is still living and 100%  involving in her life!………Will Zari disappoint many or will she continue to shine and come-out as a shero? Will this be Zari’s downfall as she may lose some sort of “respect” from Ugandans who are / were hardcore fans of the “Rich Gang” particularly  The Don- Ivan Ssemwanga?! Will Watanzania accept Zari and give her 100%  support to carry their flag as Diamond’s wife especially after his bizarre behaviors of abusing and disrespecting women!?! Remember “The B**** is dying for fame”  and “the baby is not mine”! And finally, the boys are growing up, one day they will have bunch of questions to ask! How will her children feel? Will they feel a sense of betrayal from their own mother; the only living parent?! Can’t get any better than this!! I will surely keep up with the story. And You be the judge!

 

“Naamini bado nina nafasi kwenye moyo wako please usiniangushe”!

Umeshawi kumpenda mtu asiyekupenda? Well, naamini wengi tu imeshawatokea. Pengine utakuta kama ni mwanamke basi anakubali hata kuwekwa kimada miaka nenda rudi basi tu mlimradi naye aseme nipo kwenye “relationship” au “married” ?? hiyo yote nikupenda asiye kupenda. Nawengine ndio wanakuwa na ujasiri zaidi kama huyu mrembo Teddy!  Jamani hii siyo hadithi ya kutunga, ni kitu cha kweli kabisa. Teddy Lacoste ni binti mzuri sana, na mchakarikaji. Kwakweli ametokea kumpenda kijana Tuma. Kwa bahati mbaya Tuma anampenda Teddy kama rafiki tu / kama dada. Lakini Teddy anaona kuwa yeye na Tuma ni “soul mate” match made from Heaven! Hivyo amekuwa akimbembeleza Tuma wawe pamoja naikiwezekana waoane wawe mke na mume wazae watoto! Ameshakuwa akimbembeleza Tuma kwa zaidi ya miaka 2 sasa kwa kutumia lugha zote za mapenzi, in private lakini ikashindikana. Sasa akaamua kuja public kwa social media. Yani ni anapost picha na status za kumuomba Tuma amkubali #Live lakini Tuma kagoma!!   Tuma ni kama mdogo wangu, age mate na wadogo zangu, amekuwa nikimuona pale mtaani kwetu KJ. Hivyo amenizoea ananiita dada. Sasa, mwaka jana mie nikaona Relationship status ya Teddy kwa Facebook kuwa “engaged to Tuma” na picha ya pete. Halafu na Tuma aka “Like” hiyo status. Basi mie nisifurahi  nikaja ipost humu (somahapa) si ndio Tuma anakuja niambia kuwa it’s not true haja mu-engaged ni vituko vya Teddy ?? mbona yalinishuka, nami nikagoma kuiondoa kwani yeye Tuma huwa ana “LIKE” hizo status za Teddy!  Sasa jana nikamwambia Tuma kuwa leo nakuja kuanika hii story yao kwa blog ili watu wengine watoe ushauri wao. Kwani mie hiyo kesi ilinishinda pale Teddy alipoileta kwangu mwaka jana. Nilimwambia mapenzi ya kutongozewa au kulazimisha mtu hayanaga mema mengi! Nimeona wengi huwa hawana furaha ya kweli. Ni shida. Hivyo yeye mwenyewe ndo itabidi aendelee kum #Seduce Tuma mpaka aukubali wimbo ?? Though moyoni natamani kama wangekuwa pamoja. I love both of them ?? ……. Haya wewe una ushauri gani kwa Teddy na Tuma?

The Untold: Siku 30 kwenye koma, jela miezi 27, na madawa ya kulevya!?!

Wahenga wanasema ukiona kwako kwaungua basi jua kwamwenzio kwa teketea! Yani kama wewe unafikiri unamatatizo au umepitia shida na vizingiti katika maisha basi kajaribu kummwambia jirani yako akusimulie yakwake! Utabaki mdomo wazi! …….Embu sikiliza history ya maisha ya Wasia Maya jinsi alivyokuja hapa Marekani, mambo yalimkuta na mitihani aliyopitia utachoka mwenyewe! Kuna wakati alikuwa kwenye koma kwa siku 30, kafungwa jela kwa miezi 27, na tamaa ya kufanikiwa kwa njia za mkato ambazo zilipelekea kutaka kuuza madawa ya kulevya!

Yani the devil! Wewe mwenzio katoka kutumikia miezi 27 jela bado tu unamuweka kwa wishawishi vya madawa ya kulevya?!! Lakini kama roho wa Mungu bado yupo ndani yako kwakweli hawezi kukuacha ukaangamia. Atakugusa kwa mguso wa pekee ambao utatosha kubadili njia zako!

“Sasa nina amani……… Nipo comfortable with my life”! Hongera sana kaka Wasia Maya, najua hii story yako itagusa vijana wengi na kuangalia maisha katika njia tofauti. Ubarikiwe sana.

“We need to be able to tell our own story…….we need to rebrand Africa”~~~~Akon

 

Jamani msinicheke, yani mie my brain ipo very “selective” inapokuja kwenye vitu vya kusikiliza, kutazama, au kukaa…….. Ubongo wangu ukigoma kuwa that’s not for you, basi inatuma msg kwa  hisia / feelings zangu nazo zinagoma kabisaaaa! Ndio maana nasema msinicheke nikiwaambia kuwa leo hii ndio kwa mara ya kwanza namsikia huyu mwanamuziki maharufu aitwaye Akon  kwasababu ni nadra sana utanikuta nikisiliza  hiyo aina ya music anayo imba! Hivi unajua sijui hata wimbo mmoja wa Kanye West ?? at least Jaz najua ule wa “All I need in this life of sin its me and my girlfriend” ?? Sasa kama na wewe ni kama mimi ngoja nikwambie kwa kifupi tu kuwa Akon ni mwanamuziki Mmarekani ambaye asili yake anatoka Senegal. Alizaliwa Marekani, wakarudi Senegal na wazazi wake mpaka alipofika umri wa miaka 7 akaridu U.S.A tena. Lakini pamoja na kuwa maisha yake yamekuwa hapa U.S.A roho yake bado ipo Africa na anataka tuitengeneze Africa yetu iwe kama mataifa hayo makubwa kwani inawezekana. Na jambo kuu la kwanza ni kuanza ku “rebrand” Africa kwa kutumia Waafrica, kulingana na maadili yetu, matamanio yetu, na mtazamo wetu! ………..tafadhali msikilize vizuri kwenye hii video ? kama lugha ni changamoto basi tafuta mtu akusaidie kukueleza…………. kusoma zaidi juu yake na malengo yake nenda ?? (Akon_Africa)

Kagua ATM yako kabla ya kuweka card!

Kuna hivi vifaa vimeingia ambavyo mwizi wa kwenye ATM anaweza chomeka na kusoma maelezo ya siri ya card yako na kuchukua pesa bila wewe kujua. Nikifaa ambacho wanakiegesha kwa juu, hivyo kabla ya kuweka card yako kwa ATM  hakikisha umekagua kwa kuvuta kidogo ule "mdomo"ambao card yako inaingia ukiona inacheza basi jaribu kuvuta kwa nguvu kidogo ili ukichomoe. Pia jaribu  kujijengea tabia ya kukagua mazingira ya ATM kabla ya kufanya kitu chochote kwani kuna wezi wengine wanategesha camera kwa juu ambazo zinauwezo wa kusoma number zako za siri. .......Tazama video ?

Special thanks to Gloria kwa ku share nasi hii video ?

“Mambo ya kuishi kwenye lijumba halijaisha na Friji limejaa maji HAPANA! not for me!” – le Mutuz Nation

EXTRA LIVE STRAIGHT TALK:- Nimesikia maneno mengi sana ya kujaribu kubadilisha Hoja yangu ya Msingi kuhusu kujenga nyumba ninasema tena kujenga nyumba ni jambo Muhimu sana na Bora sana ila kujenga Nyumba kama Elimu huwa sio la kila mtu kuna wanaotakiwa kulifanya lakini sio wote na inatokana na MIPANGO KWANZA .........Kwa bahati mbaya sana Wabongo tumeliweka hili la kujenga mbele sana mpaka tunaishia kushindwa kuishi Maisha yetu mpaka tunashindwa ku enjoy our lives kisa kujenga tu that I am against ...

Kama ni mfanyakazi ili ujenge nyumba unatakiwa upate mkopo na ni lazima uwe na kazi nzuri yaani umesoma vizuri so unaweza kuutumia ujira wako kwa maisha na kubakisha akiba ya kujenga smoothly sio kukosa maisha watoto wako wanateseka kisa kujenga nyumba HAPANA! ...na ndio hizo nyumba sasa hivi zinauzwa kila kona tena kwa bei poa kisa wenye majumba walikuwa wapiga dili Makazini sasa toka Magufuli awe Rais hamna madili tena mshahara hautoshi unaanza kurudi tena ulikotoka na ambako ndiko you belong kupanga kitu ambacho ulitakiwa kutumia akili mapema sana ukaenda na maisha pole pole ...

Kwa mfano mimi nilijenga nyumba nikiwa Majuu baadaye nilipokuja kupata akili ile pesa ningeweza kununua nyumba Majuu nikaiuza kwa pesa ndefu sana wakati nimeamua kurudi bongo ningeweza kujenga nyumba hata Tatu kwa pesa ile ile ambayo sasa hivi imekaa tu pale Kinyerezi for nothing ...now kuna Elimu yako na ya Watoto ambayo n muhimu sana kuliko hata Nyumba si mnawaona watoto wa wenye nyumba mlizopanga hela za kodi hazitoshi kwa mwenye nyumba kuishi vizuri na familia yake wanaishia kukimbizana na Wapangaji kuongeza kodi kila siku .... Again ninasema kila mtu na maisha yake ila mimi binafsi nitaendelea kukaa nyumba ya kupanga hapa Downtown huku nikiendelea kuwekeza na kujenga Nyumba mpya Mbweni na nitaachana na ya Kinyerezi lakini siwezi kujinyima maisha yangu kisa kujenga nyumba Mbweni HAPANA! no way ...nitapigana na maisha kupata mapato ya kutosha kuishi vizuri sasa hivi as I do and then nitaangalia kama zinatosha akiba ya kujenga pole pole lakini cha msingi ni kwanza kuishi maisha mazuri sasa hivi mambo ya kuishi kwenye lijumba halijaisha na Friji limejaa maji HAPANA! not for me! - le Mutuz Nation

“He picked me up from baby daddies cave”-Akothee Akothee

Akothee Akothee back in 2013

He picked me up from baby daddies cave , asked me to throw away my jacket which looked cheap for him , alas,  that was my sunday best! So he gave me his own jacket,  I had piecings on my nose, my cheek & many other places ??? he asked me to take them out. I asked why & so many whys? He said (you are a natual beauty,  you don’t need any additional metals on your dark flowless skin,  &, I want to have a lady on my table) ??, He  immidiately  took me to a shopping center & changed my wardrobe before he introduced me to his friends. He held my hands & walked into some exclusive restaurant where his friends were , with his head high in the sky, he said;  meet my sweetheart Esther Akoth! So with all these imistakes from my dress code to pieciengs this guy still insisted on dating me,  why do you think he was patient with me till he found the lady he wanted in me? Was he walking with a microscope to see the inner beauty? I still make so many mistakes till todate he has never given up on me! I call him Dr. K . his patience is unlimited, he is waiting for me to drop music so we can get married….. Dr. k , its soon dont worry;  I love you very much ???? you try tell him anything negative about Esther he deletes your contact & thats the end of your relationship ??? #TB2013

****Please note, this msg is #TB2013, Akothee has been married to her man at least for 3yrs now! May their ❤ forever live ****

Soma maoni ya watu / fans:  

Kama “Boaz” angeambiwa achague mwanamke katika dunia ya leo…..!!

 Embu tucheke kidogo maana hii weekend ndefu hapa U.S.A kwasababu the Independence ya Marekani ni JumaNne!……… Basi kama ilivyo, nimekwenda kwa Instagram ya #Askcheyb nakukutana na hii topic ya wadada kuvaa nguo karibia na nusu uchi! Eti anasema kuwa kama “Boaz” wa kizazi kile cha kwanza angekua ndio anatafuta mke katika karne hii 21 ambapo wasichana wengi wanatembea nusu uchi kila siku mida yote; ingekuaje? Muandishi wa mada anasema wanawake wa namna hiyo wapo kwaajili ya “mburulaz”!  Labda nikukumbushe kuwa muandishi ni mtaalamu wa mambo ya mahusiano!~~~~~ embu jisomee mwenyewe ??

Could you imagine “Boaz” choosing some of these chicks who parade half naked on IG ALL  day everyday? Nah, them chicks are for “Dumbaz” ??” Sasa mimi nashindwa kuelewa kwani jambo kama hili lingeandikwa na “Muafrika” kutoka Africa nisinge shangaaa sana. Lakini huyu ni Mmarekani mweusi ambaye amezaliwa na kukulia hapa Marekani! Watu kutembea nusu uchi hapa Marekani nikitu cha kawaida sana. Sijui tatizo nikuweka hizo picha kwa Social media au ni nini! Kwamfano, mtu kama Oprah aliwahisema kuwa siku ukikutana na picha ya yeye amevaa “bikini” au swimsuit basi jua kuwa ni fake! Kwani hata siku mmoja haitokaa itokee yeye kuvaa hivyo kwa public! Lakini unakuta watu kama wakina Michelle Obama wao wapo free kuvaa swimsuit mbele za watu japo hukuti akizipost picha hizo kwa social media isipokuwa  ma-paparazzi huwa hawapitwi na jambo! ~~~~ Sijajua kwakweli inakuaje watu walio zaliwa kwenye mila na tamaduni sawa wakawa na mtazamo tofauti wa maadili ya mavazi! Embu tujikimbushe na hii topic hapa ?? KamaMkeRaisAnawezaVaa.    

SOMA MAONI YA WENGINE!

 

 

your lifestyle & dreams will determine the kind of a man you would like to marry ~~~Akothee Akothee

fb_img_1479852575141It’s a free world , date whoever you feel like , even baboons attract tourist, as long as you are happy , then we should be happy for you, be proud of your Man /woman, we all have different tastes, ambitions, lifestyles, etc , your lifestyle & dreams will determine the kind of a man you would like to marry ??? usisumbue watu akili, gone are days when even parents would choose who you settle down with , today, they can only make noise & adjust to it . Choose your rib wisely, for when it is sweet , you won’t tell us , you will only share with us the challenges! & we will either laugh at you or do very little,fb_img_1479852719471in short LIVE & LOVE YOUR LIFE DONT LISTEN TO THOSE WHO HAVE BEEN SINGLE FOR TOO LONG , THEY ARE TOO SELFISH TO SHARE THEIR EXPERIENCES, but for sure every woman needs someone to hold, laugh, & cuddle Hakuna age kwa hizi

Wema Sepetu katika ubora wake!

Wema Sepetu katika ubora wake! Vazi limemkaa haswa aaa! Kapendeza sana! My dear Wema naomba leo nikushauri, unajuwa wewe ni our Sweetheart! Tunakupenda sana na kukutakia mema! Naomba usichukie kuhusu ushauri wangu kwani unatoka from a good place of my heart, na pia sio lazima uhufuate unaweza ukasoma na ukauwacha kama ulivyo! Na ninakuhakikishia bado nitakupenda bila kinyongo! …… Wema sikiliza: 《1》Hii karne ya 21 kuzaliwa mzuri tu haitoshi! Wewe ni mzuri sanaaaaaa! Lakini unamengi ya ku-prove ili umpate yule mume / partner unaye stahili kuwa naye KAMA KWELI HILO NI HITAJI LA MOYO WAKO!

《2》 Achana kabisa na watu /fans wako ambao saa zote wanakueweka katika muonekano wa “mashindano” na mtu fulani haswa Zari, wakati Zari got no time for nobody yani yupo busy na maisha yake! Wewe ishi maisha yako bila kupigizana kelele na mtu! Au kuweka mazingira fulani yanayo onyesha some sort of competition! Kumbuka mtu yeyote yule ambaye anataka kushindana na mtu jua huyo mtu teyari umesha mzidi ndio maana anataka aku-drug down to  his /her level! Always choose “highway” na sio mashindano! 《3》Ngoja nikwambie ukweli, wewe na Zari wote ni wazuri sana tena to be fair labda niseme wewe umependelewa zaidi na figure kuliko Zari! Hata hivyo any man ambaye ni potential au well successful will absolutely pick Zari over you! Unajua kwa nini? Zari has proven herself kuwa (a) she knows what she wants in her life! And happiness is her number one priority! Na ndio maana aliamua kuachana na marehemu Ivan Ssemwanga na kuwa na Diamond! She prefers happyness over money (b) Zari has proven kuwa she can make her man to be the best of all! She did that twice! Kwa marehemu Ivan Ssemwanga na sasa kwa Diamond! Ndio, unaweza sema ulimpenda Diamond akiwa bado “Nasib Abdul” but mdogo wangu, wenyewe wanasema hivi “a man with dreams need a woman with vision”! Na hapo ndipo Zari alipokupiga bao! You knew Nasib’s dreams but you didn’t have VISION to take Diamond where he needs to be! Plus badala ya kuwa team player ukawa kama una compete na Diamond; kumbuka zile kauli kuwa “anatembelea nyota yako” toka kwa mashabiki wako na watu wako wakaribu! Zari aliacha yote kumjenga Diamond at least for the first two yrs ya relationship yao. Building Diamond ikamsaidia kujiendeleza na yeye pia kwa ku-expand her empire in Tanzania. Wakati alionekana kama amepoteza Dira ya maisha  kwenye macho ya watu wenye mtazamo finyu lakini kwetu sisi wengine tulijua Zari is going to surprise them big time and she surely did! Kumbuka nimekwambia kuwa Zari nia yake ni kuwa na mwanaume ambaye will make her happy, and that is what exactly Diamond is doing! Spoiling her right before your eyes! Pia angalia Ivan Ssemwanga, pamoja na yote bado Zari alikuwa ndio Kimbilio na tegemeo lake! Kitu ambacho wewe mpaka dakika hii pamoja na kuteka people’s heart but none of them can trust you with their “treasure” or legacy! (c) Zari has proven kuwa she is not only a great partner but  she can hold down a family as well! She’s strong, has good family values enough to make her own family kitu ambacho wanaume wengi waliofanikiwa wanapenda kuwa nacho! Na hapa siongelei kuwa na watoto kwani watoto ni mipango ya Mungu! Ninacho kisema hapa nikuwa “grounded” enough to make someone’s house a family friendly place ambapo mtu kama Dr. Mengi atakuwa excited, and proud enough kusema I’m going home na once in a while kuwaita some of his friends for dinner! Mpaka sasa kwa hili mdogo wangu Wema, umefeli kabisa! Siku zote waliokuzunguka mmh! only God knows who they are! Embu jifunze kitu kutoka kwa aunt Ezekiel! 《4》 My dear Wema, achana na kutafuta attention zisizo na kichwa wala miguu! Don’t let them losers and fools use you my dear! Kama kweli you want to have that potential man holding your hand then you need to prove kuwa you are a woman of character! Make your man feel secured kuwa hayupo kwenye “competition” with another man! Yani kuwa akija mwenye hela zaidi yake he’s out of the league! Hii inaweza ikawa ngumu kunielewa lakini mpaka utakapo elewa hichi ninacho kwambia basi tegemea kutumika na wanasiasa pamoja na wenye pesa za “mission-town” ambao wanatafuta kuandikwa kwenye magazeti ya udaku!

《5》 Kama nilivyo sema kuwa you’ve  a lot tu-prove na kitu kingine ni kuonyesha kuwa you can stand strong alone na kua-achieve something for your own good! Kwamfano mimi sio such a “career woman” but I managed to get my college education. Nasio hivyo tu, nimelea mwanangu ambaye niko so proud of her! Plus, naishi mwenyewe hapa Marekani bila msaada wa mwanaume hivyo mwanaume yoyote yule atajua kuwa kama tumependana ni kwasababu zingine na mapenzi ya kweli nasio ugumu wa maisha wa hapa Marekani! Angalia, mfano wa karibu ni Jokate, she’s a great example kama utataka kujifunza kutoka kwake! You have to show some potentials!

《6》Lamwisho, achana na mashoga a.k.a “wadada wa mujini”! You have your sisters make them marafiki zako wa karibu. Unaweza ukawa na baadhi ya marafiki wazuri kwa kula “bata” but don’t let them be your close friends! Kwasababu naona wengi wao sio wazuri na mkikorofishana siri zako  zote wanakutolea nje wakati wewe sioni kama unatabia ya kutoa siri za watu! Hivyo achana nao kabisa! Otherwise, mie nakupenda sana na nakutakia mafanikio mema. Najua bado unanafasi ya kufanya matengenezo! Kama nimekosea naomba unisamehe sana. ❤

“Mafanikio makubwa sio wewe tu”

“They might not deserve forgiveness but you deserve your life, and that life comes through your forgiveness.”

Don’t confuse all the healthy masks with healthy Christians. Many are suffering in silence or stuck in a history hurt. It’s not what happens to us, it’s what happens in us that keeps us stuck in pain. The event is passed, but we’re not released from the internal damage caused by what happened when we’re unable to grow forward.

I love Jokate’s pic……has nothing to do with the story

Growing starts with acceptance — pain will come, people will do wrong. Accept that fact. They might not deserve forgiveness but you deserve your life, and that life comes through your forgiveness.

Second, we have to acknowledge what we learned from it — when we follow and focus on the lesson, the pain will eventually leave. Pain relies on our focus on the problem, instead of the lessons learned. When we let pain consume us, we push out faith, hope, joy, and potential.

Remember, pain is what happened because of what happened, misery is what we do to ourselves because of what happened. But your destiny is too important to live stuck in what happened.~~~~C&P from Bishop Larry Facebook page

Niliwahi kusema hivi………!

“Ok! Lemme today address this issue to my fellow friends who think someone is less of LADY/WOMAN unless you wear something under size 10 or you have to look a certain way. First of all, we all are human being regardless of how we look-created by one person we call Him God, and to Him we all shall return one day.

Second, woman is woman whether she is fat or skinny, rich or poor, famous or not famous, tall or short, hair or hairless, black or white. We are all women and no one is obligated to be or do anything other than what they choose to be!! Third, to those people who constantly telling me “umenenepa sana, unabidi upungue” well, we all have had different life experiences and our bodies react differently, that doesn’t make any of us less woman. I do understand about health issue but who told you I’m not healthy anyway?! And where is written that skinny people are the most healthiest people in this planet?! Btw being healthy isn’t something I owe anyone except myself!! I don’t have to adhere to anyone’s specifications to be a valid woman that God has created me!! So please, save those comments “unabidi upungue” to your mama!! Yes, I said to “your mama” as I’m someone’s MAMA, she loves me, respects and adores me the way I am!!! Finally, if it’s true “we are what we eat” then I think some people need to eat BIBLE to Detoxify their evil ugly hearts!! #KeepingItReal” ******This is a Repost from my Facebook 2014**** ujumbe wangu kwa wanawake wote kuwa you are beautiful they way you are!! Don’t let idiots make you feel like you’re less of woman just simply you can’t wear size 8!! Confidence is the best outfit, keep it on everyday, and real beauty comes from within sio kwenye size ya nguo yako!! Umeshawahi ona mtu anavaa size 4 lakini anaroho ya kishetani!! Yani sura yake na matendo yake represent nothing but a devil?! I mean, am just saying!!……Wataalamu wanasema kuwa “big girls they always got big hearts”!!

Love conquers all!

Huwezi kumuonyesha KIPOFU NJIA  kwa kumtembeza gizani kwani yeye ni kipofu na haoni kama yupo gizani!! Huwezi kumfundisha mtu ambaye ni “bully” kuacha ku-bully watu just by doing the same thing wakati hicho ndicho anachokijua na ku- experience in his / her whole life!! Love! Love! Love! Kama Yesu alivyo tupenda sisi nasi tupendane vivyo hivyo!! Love conquers all!…………Kwa msionifahamu mimi naitwa Alpha Igogo na Upendo ndio Dini yangu! Nasema hivi My name is Alpha Igogo and Love is my Religion! Mbarikiwe wote.

“Don’t make marriage a jail”~~~ChrisMauki

Enyi waume, wake zenu pia ni wanadamu, they are social beings, walikuwa na marafiki kabla hamjawaoa, usidhani wewe ndio ulikuwa binadamu wakwanza kwenye maisha yake. Kasoma kuanzia shule ya awali hadi chuo kote ana marafiki au hatakama hajasoma lakini ana marafiki wa mtaani na ujanani. Iweje leo kaolewa na wewe ndio unajifanya kumfungia kila mwanya wa kuonana na marafiki zake (simaanishi marafiki wa mapenzi), unamkataza kutoka, akienda vikao vya kinamama ni shida, akijiunga vikoba ni shida, akitaka kwenda kwenye mikutano ya dini ni shida kubwa, unamyima kuwa na marafiki na akitoka kidogo basi hauishi kupiga simu kumuuliza anarudi sangapi. Ikifika saa 12 jioni utaskia mwanaume anamwaga povu “wemwanamke uko wapi, wehujui ni mke wamtu? Unafanya nini nje hadi sahizi”? Mimi nikuulize, kwani wewe haujui kuwa wewe ni mume wamtu na baba wa watu? Sasita usiku unafanya nini nje ya nyumba? Au umekuwa jambazi? Simaanishi akichelewa asiulizwe la hasha, namaanisha kunyimwa uhuru kusipitilize ikawa utumwa, kisa eti wewe haupendi awe na mahusiano na wengine. Mwanamke hajaolewa na wewe kuja kuua ulimwengu aliowahi kuwa nao awali. Lets be fair to each other. Ni vizuri kilammoja akijali hisia na wellbeing ya mwenzake, na hapo ndipo furaha ya kuishi pamoja inapokuja. Dont make marriage a jail #ChrisMauki

“Your life is your right. Never give the control of your life to anyone in life”

Some people are already troubled, looking for who to trouble. A person who is always looking for people’s trouble everywhere is internally troubled. The dream of a sadist is for everybody to be miserable in life. A negative person is always looking for who to fight, they always find fault in everything you do and then make you feel like you’re the bad person. A sadist always look for a place to transfer or dump his/her frustration. Never allow anyone to make you feel guilty for their own misfortunes. You may not have control over what people bring to you, but always be in control of what you take from them. Never allow anyone to take your happiness from you. Once they manage to frustrate you, they already have the power to control your emotions. Whoever controls your emotions, controls your sadness and joy. Your life is your right. Never give the control of your life to anyone in life. #akininspiration

Mama Salma Kikwete umekosea sana! Hiyo inaitwa institutionalized discrimination!

Mama yangu, ninacho jaribu kukwambia ni kwamba fungua macho yako utazame hii hoja yenu kwa macho mapana utaona jinsi gani imejaa ubaguzi na unyanyapaaji wa hali ya juu kwa mabinti wanao pata mimba wakiwa shuleni! Kama mmeamua kufukuza shule wanafunzi basi mfukuze wote wanaofanya ngono wakike na wakiume kwa ujumla wao na siyo kubagua wanaopata mimba tu! Hivi mama Salma, kweli unataka kusimama hapa na kuiambia dunia, mbele za Mungu kuwa huyu binti yako mwenye gauni jeusi bado ni bikira?! Au kwasababu hajapata mimba kwahiyo unamuona mtakatifu?!! Kumbuka kabla ya kutunyooshea kidole sisi hakikisha kucha zako ni safi! Maana lazima tutazikagua!! Hizi sheria mnazoziweka bila kutafakari madhara yake katika jamii ipo siku damu zenu zitazilipa tu! Yawezekana leo hii haitamkuta binti yako lakini huenda kesho yakamkuta mjukuu wako! Oh! Nimekumbuka nyie ni “high profile” people, you do “high profile crimes” bila sisi walalahoi kujua, mama kumbuka Mungu anawaona!!

Kumnyima mtoto yoyote haki ya ku-access education ni kinyume na haki za binadamu. Kwani kupata elimu ni haki ya msingi ya binadamu wote! Wanafunzi wanaopata mimba wanatakiwa waachwe waendelee na masomo yao kama kawaida bila kubaguliwa na mtu yoyote yule. Kama hiyo ni ngumu basi wapewe “sick leave” wakisha jifungua waendelee na masomo yao.  Au kama hizo mimba zinawakera sana basi wafungulieni Abortion clinics ili wawe wanakwenda kuzi-abort huko, labda roho zenu zitafurahia!!

Kumbuka kuwa unapomnyima mama moja  haki ya kuelimika inamaana unatengeneza jamii / community ya watu wasio na muelekeo wa maisha na kuendeleza mila ambazo hazina tija kwa taifa! Mama ndio nguzo za familia nyingi haswa Africa. Hakuna njia mbadala katika hili swala zaidi ya kuwaacha waendelee na masomo yao bila ubaguzi wowote ule kwa faida zao binafsi, vizazi vyao, na taifa kwa ujumla!

Ngoja nimalizie kwa kusema kuwa, tatizo wazazi wengi wa Africa wanataka waonekane kuwa wao ni malaika hawajawahi fanya mistakes yoyote ile maishani mwao! Ndio maana wako guilty na busy kuwahukumu watoto kwa kuwapa adhabu za ajabu ajabu badala ya kuwaelekeza juu ya maisha. Unajua yale mambo ya kila mzazi anajifanya alipata ‘A’ darasani, alikuwa wakwanza siku zote, na kila mwanamke aliolewa akiwa bikira! Just a bunch of nonsense (Excuse my language)!. Uongo mwingi kwa watoto zenu bila sababu yoyote ya msingi!  Btw, hii ni karne ya 21, mama yangu where have you been?! Unaona statistics za dunia zinavyo kwambia yani karne hii wazazi nmnatakiwa kuongea na watoto / wajukuu zenu juu ya sex / elimu ya kujamiiana kabla ya miaka 10! Kwani watoto wa miaka 10 siku hizi wako sexually active na wengine wanabeba mimba! How? I don’t know usiniulize mimi lakini hiyo ndio hali halisi ya sasa, just get with the program mama!!