Category Archives: politics

HUU NI MWAKA WA KUONGEZA NA KUTENGENEZA MAHUSIANO MAZURI NA WANA WA NCHI WA TANZANIA- Peter Sarungi

Kila mwaka una lengo kuu endelevu linalotimizwa kuanzia mwanzo wa mwaka hadi mwisho wa mwaka. Kwa mimi Simba wa Utegi na Babu wa Kagera nimeamua kuweka mwaka huu 2017 kuwa mwaka wa kutengeneza mahusiano ya kijamii, kisiasa na kiuchumi na wananchi. Mahusiano yanatengenezwa kwa kupitia mawasiliano.

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

Unaweza kunipata kupitia:

1. Public No & Watsup No. +255 713 037 798

2. Facebook ID : Peter sarungi

3. Instagram ID : peter.sarungi

4. E. Mail : [email protected]

5. Tweeter ID : @psarungi

6. Post Code : 9291- Dar es Salaam

7. Physical Adress : Chanika Village – Dar

Hizo ni baadhi ya njia unazoweza kunipata kupitia mawasiliano yangu rasmi kama Next Speaker mwaka 20…

Karibu tuwasiliane katika kujenga nchi ili hata watoto,wajukuu,vitukuu na vizazi vijavyo vije vipate kula matunda yetu

Imetolewa na:

Idara ya Habari na Maelezo ya Peter Sarungi

Raisi-Jukwaa la Walemavu Tz, Next Speaker. Asante sana kaka yangu mimi pia nitakuwa mmoja wa wafuasi wako!

2016 ULIKUWA NI MWAKA MGUMU SANA ULIOKUWA NA MABADILIKO YA GHAFLA YA JPM by Peter Sarungi

Ni desturi yangu kutathmini mwaka unapofikia mwisho. Nianze kwa kuimba wimbo wangu kwa Tanzania.

“Tanzania eeee, Nakupenda sana x2”

“Hata kama nikilala porini lakini ni ndani ya Tanzania bado nitajivunia”

“Najua wengi wanakutamani ingawa uchaguzi wako bado upo mashakani”

“Nakuaga mwaka kwa maumivu ingawa ni maumivu ya mpito”

“Naamini sasa ni muda wa kula matunda ndani ya mwaka unao anza”

Kwa kifupi mwaka 2016 ulikuwa ni mwaka mchungu na mgumu kwa watanzania masikini na wanyonge wasio jua leo yao itakwishaje na kesho itaanzaje baada ya kuletewa utaratibu wa kufanya kazi kabla ya kula ingawa kazi zenyewe hazipatikani na zingine zinezuiwa kupisha uchunguzi wa HEWA.

Ni mwaka uliokuwa mgumu kwa watumishi wa umma baada ya kulazimishwa mabadiliko makubwa ya utumishi wa serikali na hasa baada ya kuziba mianya mikubwa ya ubadhilifu wa pesa za umma pamoja na kuziba hadi vitundu vidogo vya posho kwaajili ua motisha ya watumishi.

Ni mwaka mgumu kwa wana siasa feki walio ingia kwenye siasa kwa maslahi ya kutajirika. kuna wabunge na madiwani walio tumia nguvu nyingi kupata uongozi, kwa sasa wanajuta ni kwanini walichagua siasa na wengine wana lia hadharani bila kuficha. Lakini pia ni Mwaka mgumu sana kwa wapenda mabadiliko, wana harakati na wapenda demokrasia baada ya kusitishwa kwa shuguli zao za siasa za majukwaa na harakati zingine kama maandamano.

Ni mwaka mgumu sana kwa uchumi wa taifa na wananchi hasa baada ya kutanda kwa UKATA wa hali ya juu sana. imefika mahala ambapo heshima ya ndoa imerejea, heshima ya mshahara imerejea, heshima ya mlo imerejea na hata heshima ya kazi imerejea. Ukuaji wa Uchumi wa nchi kwa mwaka huu nimeufananisha kuwa na kasi  kama ya konokono dhidi ya farasi. Naamini imekuwa hivyo kwa sababu JPM ametumia mwaka huu kuweka misingi sawa, tuangalie mwaka 2017

Umekuwa ni mwaka wa Matamko mbalimbali machungu kwa wanchi katika sekta mbalimbali. Tumepata matamko mengi ya wakuu wa mikoa mbalimbali hasa Dar, matamko ya wakuu katika Mfumo wa Elimu, Afya, Ardhi, Kodi, Usafirishaji, kilimo, Ufugaji, bomoa bomoa, Madini, Umeme na maeneo mengine yaliyo acha alama ya maumivu kwa wananchi.

Tumeshuhudia hadithi za mfalme Juha na simuzili za kusadikika kutoka kwa Polepole, Ben sa8, Yericko nyerere, Faru John, Magoiga, Menuka, Malisa na wengine wengi waliokuwa mstari wa mbele kutupigia hadithi nzuri kwa kila upande kwa mwaka mzima.

Ulikuwa ni mwaka mchungu sana kwa watumishi wa umma zaidi ya 300 walio tumbuliwa mwaka huu kutokana sababu mbalimbali kupitia kauli mbiu ya KUTUMBUA inayoongozwa na mkuu wa kaya akisaidiwa na wasaidizi wake kila idara.

Ulikuwa ni mwaka mchungu sana kwa wafanya biashara za utalii, mahoteli, mabasi, nguo, bar, ujenzi, usafirishaji wa mizigo, wamachinga, madalali, vyuo na mashule, biashara za mitaji na biashara za Bank. Maana tumeshuhudia taatifa za kufilisika kwa baadhi ya biashara hizo kwa sababu ya mdororo wa uchumi. Tusife moyo, mwaka ulikuwa ni wa mapito.  

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

#MyTake

Mwaka umekwisha na changamoto zake, ikiwa mwaka unao anza utakuwa na changamoto hizi basi tujue ni sisi wenyewe tutakuwa tumezitengeneza. Huu ulikuwa ni mwaka wa majaribio ya mabadiliko makubwa, naamini tutajipanga sasa kukubali na kukabiliana na magumu yanayotokana na Mabadiliko haya kutoka kwa Mkuu wa Kaya…….Mwaka 2017 ukiwa mchungu tena kwako basi jua ni kati ya wewe au serikali kuna mmoja atakuwa ni mzembe wa mabadiliko.

Kumbe na huyu ni shemeji..!

Kumbe na huyu kimbau mbau mwiko wa pilau ni shemeji yangu ?? Yani wewe Max ndio unasumbua kichwa ya baba yangu Dr Magufuli na #FreedomOfSpeech? Utafikiri unaijua vile ??? Kama  kweli wewe unapigania hiyo “huru ya kujielesa”  (in Luo’s voice)   mbona siku ile yule “mwanaharakati” nyenzio alianika wewe na familia yako aka bandika na picha ya mutoto yako kwa mtandao yake ulipiga magoti yako kwa nguvu sana ukaomba msamaha akutoe kwa blog yake nakuwa hauto rudia tena kumuongelea??? Kwani hile haikuwa #FreedomOfSpeech ??  Au nyie hii ya kwenu  ina “discrimination”?? ????? •••••• Anyway pole kwayalio kukuta binafsi sipendi kuongelea mambo ambayo yapo Mahakamani kwani tuache Mahakama zifanye kazi zake bila kuingiliwa na mtu yoyote kwa uhuru na uwazi! Lakini hata hivyo naamini haya yataisha na punde utakuwa huru! And you and your #FreedomOfSpeech can go away ???

 

“It’s time to change our political culture”

Sent as received. However, I still have so many questions and am yet to get answers. So many sayings come to my mind:
1. If it’s too good to be true probably it is not
2. There is no free lunch
3. Not every kiss represents love, think of Judas when he betrayed Jesus
4. Change begins with me
5. If I can dream it I can achieve it

The list of thoughts is endless. Looking forward to reading different perspectives and probably solutions

Every Patriot in Africa should read this article; penned by US-based Zambian media practitioner and author. He is a PhD candidate with a B.A. in Mass Communication and Journalism, and an M.A. in History.

They call the Third World the lazy man’s purview; the sluggishly slothful and languorous prefecture.

In this realm people are sleepy, dreamy, torpid, lethargic, and therefore indigent—totally penniless, needy, destitute, poverty-stricken, disfavored, and impoverished. In this demesne, as they call it, there are hardly any discoveries, inventions, and innovations.

Africa is the trailblazer. Some still call it “the dark continent” for the light that flickers under the tunnel is not that of hope, but an approaching train.

And because countless keep waiting in the way of the train, millions die and many more remain decapitated by the day.

“It’s amazing how you all sit there and watch yourselves die,” the man next to me said. “Get up and do something about it.

When I first discovered I was going to spend my New Year’s Eve next to him on a non-stop JetBlue flight from Los Angeles to Boston I was angst-ridden.
I associate marble-shaven Caucasians with iconoclastic skin-heads, most of who are racist.

“My name is Walter,” he extended his hand as soon as I settled in my seat.

I told him mine with a precautions smile.

“Where are you from?” he asked.

“Zambia.”

“Zambia!” he exclaimed, “Kaunda’s country.”

“Yes,” I said, “Now Sata’s.”

“But of course,” he responded. “You just elected King Cobra as your president.”

My face lit up at the mention of Sata’s moniker. Walter smiled, and in those cold eyes I saw an amenable fellow, one of those American highbrows who shuttle between Africa and the U.S.

“I spent three years in Zambia in the 1980s,” he continued. “I wined and dined with Luke Mwananshiku, Willa Mungomba, Dr. Siteke Mwale, and many other highly intelligent Zambians.” He lowered his voice. “I was part of the IMF group that came to rip you guys off.” He smirked. “Your government put me in a million dollar mansion overlooking a shanty called Kalingalinga.

From my patio I saw it all—the rich and the poor, the ailing, the dead, and the healthy.”
“Are you still with the IMF?” I asked.

“I have since moved to yet another group with similar intentions. In the next few months my colleagues and I will be in Kenya to hypnotize the Raisi

I work for the broker that has acquired a chunk of your debt. Your government owes not the World Bank, but us millions of dollars.

We’ll be in Lusaka to offer your president a couple of millions and fly back with a check twenty times greater.”

“No, you won’t,” I said. “King Cobra is incorruptible. He is …”

He was laughing. “Says who? Give me an African president, just one, who has not fallen for the carrot and stick.”

Quett Masire’s name popped up. “Oh, him, well, we never got to him because he turned down the IMF and the World Bank. It was perhaps the smartest thing for him to do.”

At midnight we were airborne. The captain wished us a happy 2015 and urged us to watch the fireworks across Los Angeles.

“Isn’t that beautiful,” Walter said looking down.

From my middle seat, I took a glance and nodded admirably.

“That’s white man’s country,” he said. “We came here on Mayflower and turned Indian land into a paradise and now the most powerful nation on earth.
We discovered the bulb, and built this aircraft to fly us to pleasure resorts like Lake Zambia or lake Kenya .
I grinned. “There is no Lake Zambia or lake Kenya
He curled his lips into a smug smile. “That’s what we call your countries . You guys are as stagnant as the water in the lake.

We come in with our large boats and fish your minerals and your wildlife and leave morsels—crumbs. That’s your staple food, crumbs.
That corn-meal you eat, that’s crumbs, the small Tilapia fish you call Kapenta / omena are crumbs.
We the Bwanas (whites) take the catfish.
I am the “Bwana” and you are the “mtu”.
I get what I want and you get what you deserve, crumbs. That’s what lazy people get—Zambians, Kenyans , other Africans, the entire Third World.”

The smile vanished from my face.
“I see you are getting pissed off,” Walter said and lowered his voice.

“You are thinking this Bwana is a racist.
That’s how most Zambians , Kenyans respond when I tell them the truth.
They go ballistic.
Okay. Let’s for a moment put our skin pigmentations, this black and white crap, aside.

Tell me, my friend, what is the difference between you and me?”

I said
“There’s no difference.”

“Absolutely none,” he exclaimed. “Scientists in the Human Genome Project have proved that. It took them thirteen years to determine the complete sequence of the three billion DNA subunits.
After they were all done it was clear that 99.9% nucleotide bases were exactly the same in you and me.
We are the same people. All white, Asian, Latino, and black people on this aircraft are the same.”

I gladly nodded.

“And yet I feel superior,” he smiled fatalistically. “Every white person on this plane feels superior to a black person.
The white guy who picks up garbage, the homeless white trash on drugs, feels superior to you no matter his status or education.
I can pick up a nincompoop from the New York streets, clean him up, and take him to Lusaka and you all be crowding around him chanting muzungu, muzungu and yet he’s a riffraff.
Tell me why my angry friend.”

For a moment I was wordless.

“Please don’t blame it on slavery like the African Americans do or colonialism, or some psychological impact or some kind of stigmatization.
And don’t give me the brainwash poppycock. Give me a better answer.”

I was thinking.

He continued. “Excuse what I am about to say. Please do not take offense.”
I felt a slap of blood rush to my head and prepared for the worst.

“You my friend flying with me and all your kind are lazy,” he said. “When you rest your head on the pillow you don’t dream big.

You and other so-called African intellectuals are damn lazy, each one of you only going for leadership; just to fill their own stomach and steal from poor.

It is you, and not those poor starving people, who is the reason Africa is in such a deplorable state.”

“That’s not a nice thing to say,” I protested.

He was implacable. “Oh yes it is and I will say it again, you are lazy in your minds.

Poor and uneducated Africans are the most hardworking people on earth. I saw them in the Lusaka markets and on the street of Nairobi selling merchandise. I saw them in villages toiling away.

I saw women on Kafue Road crushing stones for sell and I wept. I said to myself where are the Zambian intellectuals? And on kenya l saw women as bricklayers. Where are these intellectual men ?

Are the Zambian or Kenyans engineers so imperceptive they cannot invent a simple stone crusher, or a simple water filter to purify well water for those poor villagers? Or sort out the drainage system to make Biogas or rivers purification systems.

Are you telling me that after thirty-seven years or more of independence your university school of engineering has not produced a scientist or an engineer who can make simple small machines for mass use?

What is the school there for?”

I held my breath.

“Do you know where I found your intellectuals? They were in bars quaffing.
I saw with my own eyes a bunch of alcoholic graduates. Calling themselves policy makers

Zambian , Kenyans , other African intellectuals work from eight to five and spend the evening drinking. We don’t. We reserve the evening for brainstorming.”

He looked me in the eye.

“And you flying to Boston and all of you Africans in the Diaspora are just as lazy and apathetic to their country.

You don’t care about your country and yet your very own parents, brothers and sisters live there.
Many have died or are dying of neglect by you as democratic government .
They are dying of AIDS because you cannot come up with your own preventive measures. To much immoral .

You are here calling yourselves graduates, researchers and scientists and are fast at articulating your credentials once asked—oh, I have a PhD in this and that so what?
What next? Handouts from IMF ? Then repay?

I was deflated.
“Wake up you all!” he exclaimed, attracting the attention of nearby passengers. “You should be busy lifting ideas, formulae, recipes, and diagrams from American manufacturing factories and sending them to your own factories.

All those dissertation papers you compile should be your country’s treasure. Why do you think the Asians are a force to reckon with? They stole our ideas and turned them into their own. Look at Japan, China, India, just look at them.”

He paused. “The Bwana has spoken,” he said and grinned.

“As long as you are dependent on my plane, I shall feel superior and you my friend shall remain inferior, how about that?
The Chinese, Japanese, Indians, even Latinos are a notch better.
You Africans are at the bottom of the totem pole.”

He tempered his voice. “Get over this white skin syndrome and begin to feel confident.
Become innovative and make your own stuff for God’s sake.”

At 8 a.m. the plane touched down at Boston’s Logan International Airport. Walter reached for my hand.

“I know I was too strong, but I don’t give it a damn. I have been to Zambia , Kenya , other African countries and have seen too much poverty.”

He pulled out a piece of paper and scribbled something. “Here, read this. It was written by a friend.”

He had written only the title: “Lords of Poverty.”

Thunderstruck, I had a sinking feeling.

I watched Walter walk through the airport doors to a waiting car. He had left a huge dust devil twirling in my mind, stirring

I remembered some who have since passed—how they got the highest grades in mathematics and the sciences and attained the highest education on the planet.

They had been to Harvard, Oxford, Yale, Massachusetts Institute of Technology (MIT), only to leave us with not a single invention or discovery.

I knew some by name and drunk with them at the Lusaka Playhouse and intercontinental hotel, safari park Kenya and Central Sports in Lusaka

Walter is right. It is true that since independence we have failed to nurture creativity and collective orientations.

We as a nation lack a workhorse mentality and behave like 13 million civil servants dependent on a government pay cheque.

We believe that development is generated 8-to-5 behind a desk wearing a tie with our degrees hanging on the wall.

Such a working environment does not offer the opportunity for fellowship, the excitement of competition, and the spectacle of innovative rituals.

But the intelligentsia is not solely, or even mainly, to blame.

The larger failure is due to political circumstances.
Knowing well that King Cobra , Kenyatta, and others will not embody innovation at Walter’s level let’s begin to look for a technologically active-positive leader who can succeed them after a term or two.

That way we can make our own stone crushers, water filters, water pumps, razor blades, and harvesters. Or dig our own boreholes without IMF involve.

Let’s dream big and make tractors, cars, and planes,
or, like Walter said, forever remain inferior…

A fundamental transformation of our country from what is essentially non-innovative to a strategic superior African country requires a bold risk-taking educated leader with a triumphalist attitude and we have one in YOU.

Don’t be highly strung and feel insulted by Walter. It is like shooting the messenger.

Take a moment and think about our country.

Our journey from 1963 has been marked by tears. It has been an emotionally overwhelming experience.

Each one of us has lost a loved one to poverty, hunger, and disease.

The number of graves is catching up with the population.

It’s time to change our political culture. It’s time for Zambian , Kenyans and other Africans intellectuals to cultivate an active-positive progressive movement that will change our lives forever.

Don’t be afraid or dispirited, rise to the challenge and salvage the remaining….

Use Africa to substitute Zambia/Zambian in the article and it holds true for all Africa/Africans.

Fact or fiction?
Just ponder.

Dr. Mwele ni hazina ya Tanzania!

screenshot_2016-12-17-02-40-34-1Ngoja niende moja kwa moja kwa mada husika! Sina hakika nalo lakini inasemekana kuwa Dr. Mwele hakufuata “protocol” na ndio maana ametenguliwa nafasi yake!……Nakubali hilo ni kosa lakini si kosa la JINAI hivyo naamini bado Dr. Mwele anafasi kubwa sana ya kutumia taifa kupitia serikali ya Dr. Magufuli kwani Dr Mwele IS ONE OF THE VERY FEW BEST ASSETS WE HAVE IN THE COUNTRY! Yani natamani nafasi ya Ummy Mwalimu itenguliwe apewe Dr. Mwele as she deserves it so very much! Watu huwa wanafanya makosa lakini kuna watu wachache sana wanaohitajika kupewa second chance na Dr. Mwele ni mmoja wao! Natumaini my baba Dr. Magufuli ataangalia hili swala kwa maslahi mapana ya taifa letu na dunia kwa ujumla!

JINSI YA KUJENGA JAMII DHAIFU NA BONGOLALA- Peter Sarungi

Nchi za Africa bado zitakuwa na kazi ngumu sana ya ki utawala katika kuunganisha jamii tatu katika nchi ambazo ni Wenye Nchi, Wana siasa na Wana Nchi ili kifikia maendeleo ya kweli. Kwa bahati mbaya kumekuwepo na udanganyifu mkubwa unao fanywa na Wana siasa walio pewa wajibu wa kuunganisha na kuleta mahusiano mazuri katika jamii hizi ili ziweze kufanya Kazi kwa ushirikiano hatimaye kuleta maendeleo ya nchi.

Wana Siasa wengi wa Africa wamevuruga nchi zao kupitia mifumo wanayoiweka katika kuongoza nchi. Wana nchi wengi bado hawajui athari za mifumo mbalimbali katika kuendesha maisha yao ya kila siku. Mifumo hii huanza kuathiri maisha ya wana nchi tangu wanapo zaliwa, ukuaji wao, kuelimika kwao, uchumi wao, afya zao, uhuru wao hadi uzee wao. Mifumo hii inaweza kuamua ni kwa kiasi gani wananchi waelimike, wapate afya nzuri, waajiriwe, wajitegemee, wapate uhuru na mengine mengi yakiwemo yanayohusu siasa. Ndio maana kuna msemo unasema ukiona wafuasi ni wabovu basi jua wametengenezwa na kiongozi wao na ukitaka kujua ubovu ama ubora wa nchi basi chunguza athari zinzowapata jamii husika kutokana na mifumo ya kuendesha nchi.

Watawala wengi wa Africa wamekuwa na uturatibu wa kutengeneza jamii dhaifu na masikini katika kuhoji, kushauri, kufikiri, wasi jitambua na wasio jua wanachokitaka. Watawala wamekuwa wakitengeneza jamii hizi ili kuendeleza malengo yao ya kutwala dola kupitia mifumo. Na kwa bahati mbaya mifumo hii imeweza kuwaathiri hadi wenye nchi na kujikuta wakitumikishwa na Wana Siasa, ndio maana utakuta kuna idadi kubwa ya wanajeshi walio ishia darasa la saba na kidato cha nne kuliko wale waliofika kidato cha sita na kuendelea. Wote hawa hujikuta wakitawaliwa na wana siasa kwa maagizo hata ya kutekeleza jambo kwa mnyonge kwa maana mfumo waliofundishwa na kuapa ni wa kutii bila kuuliza.

Watawala wengi wa Africa wameweza kupitisha na kuhalalisha mifumo ya kuzalisha jamii dhaifu na Bongolala kupitia njia tatu….fb_img_14819059905521. KUDHOOFISHA ELIMU KWA JAMII
Watawala wengi wa Africa wana amini kuwa kutawala jamii iliyo elimika kupitia Elimu bora ni ngumu sana na ina waweka katika riski kubwa ya kutawala milele, hivyo hulazimika kutengeneza jamii kubwa isiyokuwa na elimu ili kudhoofisha uelewa wao na uwezo wao wa kufikiri. Watawala hawa wana vuruga mfumo wa elimu kwa makusudi na kuweka mifumo dhaifu yenye kutoa nafasi ndogo ya wana nchi wachache kupata elimu hadi ngazi za juu na hata hao wanaopata nafasi hiyo hawapati Elimu inayostahili na kumkomboa karika utegemezi.

2. KUDHOOFISHA UCHUMI WA JAMII
Ni ukweli usio pingika kuwa Uchumi imara ni nguvu nzuri kwa jamii. Jamii yenye uchumi imara inaweza kuelimika kwa gharama yoyote ile ikiwa uchumi wao ni imara. Jamii yenye uchumi imara inaweza kuamua kufuatana na maslahi yao hata inaweza kupinga mifumo dhalimu ya nchi na hata kuwapinga watwala. Kwa kuhofia vikwazo hivyo, Viongozi wengi wa Africa wamekuwa wakidhoofisha uchumi wa jamii zao ili kuwafanya wanyonge wasioweza kuhoji ubaya ama uzuri wa watawala. Viongozi wengi wamekuwa wakikusanya pesa nyingi kupitia kodi na kujilimbikizia wao pamoja na utawala wao kama alivyofanya hayati Mobutu Seseko wa Congo. wanapenda sana kuona pesa nyingi zikiwa kwao kuliko kwa wana nchi na ndio maana hata sekta binafsi zina zorota katika kuchangia maendeleo ya jamii.

3. KUDHOOFISHA UHURU WA KUTOA MAONI
Watawala wengi wa Africa hawapendi kusikia maoni tofauti na waliyo nayo wao, hawapendi kusia ukweli walio uficha, hawapendi kupingwa kwa namna yoyote ile. Hivyo watawala hawa wataingiza sheria na taratibu za kuua uhuru wa kutoa maoni kinzani. Inaaminika kuwa kuna watu hata ukiwa dhoofika ki uchumi na ki elimu lakini bado wanaweza kiwa wajasiri wa kutoa maoni yao hata kama ni ya kupinga utawala bila kujali vikwazo walivyonavyo. Hivyo ili kuto ruhusu riski hiyo, watawala huweka mifumo ya sheria za kukandamiza Uhuru wa kutoa maoni na hata Uhuru wa kujieleza kwa jamii.

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!
Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

#MyTake
Africa kama ilivyo nchi ya kisadikika, ina safari ndefu sana ya kubadili mifumo ya nchi. Mabadiko hayo huletwa na jamii iliyovuka vikwazo vitatu hapo juu yaani lazima uwe vizuri kichwani, uwe vizuri mfukoni na uwe na njia nyingi tata za kutoa maoni yako. Kinyume na hapo itakugharimu wewe na familia yako.

Asanteni sana, ngoja niendelee kutunisha mfuko wangu ili itakapo hitajika kubadili mfumo nami niwemo.

“Haya ni maneno yake Mwenyekiti wa Chadema Mbowe”-Lemutuz

screenshot_2016-12-15-10-43-34-1screenshot_2016-12-15-10-47-27-1screenshot_2016-12-15-10-47-59-1screenshot_2016-12-15-10-48-21-1

“Guys think before you speak” -Lemutuz

screenshot_2016-12-15-10-50-57-1

“Maisha ni kupanga na kupanga ni kuchagua”-Lemutuz

screenshot_2016-12-15-10-53-22-1 screenshot_2016-12-15-10-57-02-1screenshot_2016-12-15-10-57-09-1

KABLA HATUJA STAAJABU UPOTEVU WA BEN, TUKUMBUKE NA UPOTEVU WA YERICKO 2015-Peter Sarungi

Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)
Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)

Nakumbuka kipindi cha uchaguzi mwaka jana 2015 kulikuwa na msako wa kumtafuta Yericko Nyerere kupitia mitandao ya kijamii baada ya kutoonekana katika mitandao hiyo kwa muda mrefu. Tulianzisha hash tag nyingi za kudai kurudishwa kwa Yericko huku viongozi wa juu wa chama wakikaa kimya bila kutoa katazo ama tamko lolote rasmi la kudai kada wake kupotea.

Kwa bahati nzuri uchaguzi ulivyokwisha hatimaye yericko alirejea huku akiambatana na kesi ya cyber crime. Mwaka huu kupitia andiko lake, Mh. Yericko alishindwa kuvumilia ikabidi asimulie yaliyojiri kupitia Filamu yake ya kihindi akisema kilichomkuta huko mafichoni akikimbia dola.fb_img_1481652596313Sasa na hili nalo la upotevu wa Ben linanipa mashaka makubwa….

ADUI WA TANZANIA NI WATANZANIA WENYEWE-Peter Sarungi

Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)
Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)

Inapotokea jambo fulani halifanyiki kwa mafanikio yaliyo tarajiwa basi wahusika hukaa na kutafakari ni kwa sababu gani jambo halijafanikiwa yaani maana yake wanatafuta mchawi ama adui aliye zuia mafanikio yao.

Tanzania yetu ni nchi yenye mipango mingi na mizuri na yenye kuvutia utekelezaji, nchi nyingi zimekuwa zikiiga mipango hii na kufanikiwa katika utekelezaji wake hata kuwa mfano kwa jamii za kimataifa. Chakushangaza ni pale unapo ambiwa kuwa chanzo cha mafanikio hayo ni mipingo iliyo buniwa na wataalaam kutoka Tanzania, maana utakuta utekelezaji wa mipango hiyo katika nchi ya Tanzania haiendani na wenzetu walio copy na kupaste kwao. Kwetu Tanzania utekelezaji umekuwa ni wa hasi na kuzalisha matokeo hasi kwa nchi.

Tumekuwa tukipata sera nyingi na nzuri lakini inapofika utekelezaji wake wanaibuka wana siasa wenye nguvu kikatiba kuliko watendaji na wanavuruga kabisa ule mpango kwa kuweka siasa katika utendaji na mwisho wa siku mambo yakiharibika wanasiasa wana ruka lawama na kuwasukumia rungu watendaji. Kila kitu katika nchi yetu kina endeshwa na siasa maji taka au siasa propaganda. Kuna haja ya wana siasa wetu kubadilika.

?????????? Hii ni shule niliyoikuta maeneo ya ndani ya Dodoma-Kibakwe katika jimbo la waziri wa TAMISEMI anaye simamia mipango na kampeni ya madawati katika shule zetu.fb_img_1481212567254Mmmmmmmh! ??????- Alpha

Habari nyepesi nyepesi ni kuwa Ivanka Trump ndio ata play the FirstLady role!

screenshot_2016-12-05-21-34-28-1Inasemekana ya kwamba Ivanka Trump ndio aka “act” as FirstLady kwenye uongozi wa baba yake. Nimeweka “….” kwasababu haiwezi ikafanywa official kwani kisheria hairuhusiwi lakini hiyo haimaanishi hawezi fanya hivyo. Yani anaweza akawa active kwenye maswala mengi kama mtoto wa Rais  napia kwenda kumuwakilisha FirstLady kwenye mikutano yote. Lakini hato lipwa mshahara wala benefits zozote kama FirstLady………….

Ivanka alikuwa very active kwenye campaign management team ya baba yake na sasa ni Adviser kwenye transition team ya baba yake ambapo hata kaka zake nao wapo. Vile vile inasadikika kuwa Ivanka Trump takuwa the most powerful First-Daughter in USA history!…….

Wiki hii walikuwa wanatafuta nyumba ya kununua karibu na WhiteHouse hapo DC. Nahilo ndilo linawapa watu imani kuwa nikweli she’s going to “act” as FirstLady sababu kwani Trump wana hotel ya kifahari hapo karibu na WhiteHouse na ina suite (chumba) specific for Ivanka Trump hivyo kama ni kumsalimia baba walikuwa na sehemu ya kulala na hata wangeweza kukaa ndani ya WhiteHouse!….. Inasemekana watoto wakiume ndio watakuwa wakiendelea kuendesha business zao………Anyway, time will tell!

Kitu ambacho sikujua kuwa Ivanka Trump na mme wake ni Wasabato kama mimi ? ? Ivanka alibatizwa kwenye Usabato baada ya kukutana na mumewe. Wakati mumewe ni Msabato wakuzaliwa. ……..You go Ivanka one day I will meet you ?? simnajua baba yangu ni President Dr. Magufuli ??

NIMEKUENZI FIDEL CASTRO KWA JINA LAKO-Peter Sarungi

Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)
Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)

Kuna watu hawawezi kupotea dunia kwa sababu ya alama walizoweka wakati wa maisha yao. Mmoja wa watu hao ni aliyakuwa muasisi mkombozi na raisi wa kwanza wa CUBA Fidel Castro.

Fidel Castro alifanya jambo ambalo lilifanywa na watu wa zamani waliokuwa na ujasiri mwingi, uthubuti mwingi, uzalendo mwingi, utu mwingi na maono ya kuifanya nchi yake ijitegemee. Hawa ni kizazi cha Kwame Nkuruma, Julius Nyerere, Nelson Mandela, Patric Lumumba, Samora Mashel na wengine wengi waliokuwa wakipambana katika kutimiza maono yao kwa nchi. Hivyo ndo vizazi vilivyokuwa na hisia za ukweli za uzalendo kwa taifa lao.fb_img_1480340327658Huyu Fidel ndio chanzo cha mimi kumwita mwanangu jina la FIDEL PETER SARUNGI nikimwenzi Jasiri wa CUBA. Historia ya Fidel ni kubwa na imebeba vitu vingi ingawa natamani kama mwanangu akirithi ujasiri, uzalendo, utu, uthubutu na uwezo wa kutawala. fb_img_1480257721064Mungu ailaze roho ya Fidel Castro mahala pema, yeye amekwisha maliza kutimiza maono yake na ameacha alama kwa jamii yake. Mungu atusaidie na sisi tutimize maono tuliyobeba.

R.I.P FIDEL CASTRO

“Aidha tunapenda udaku kuliko mambo ya muhimu kuhusu our lives au hatujui what should be our priorities”-Lemutuz

screenshot_2016-11-25-16-00-39-1

WALEMAVU WALIOPATA FURSA WAMEJISAHAU SANA-Peter Sarungi

Peter Sarungi (kushoto), Spika wa Bunge ndugu Ndugai pamoja na viongozi wengine wa siasa,
Peter Sarungi (kushoto), Spika wa Bunge ndugu Ndugai pamoja na viongozi wengine wa siasa,

Kuna msemo wa wahenga unasema ALIYESHIBA HAMKUMBUKI MWENYE NJA. Haya maneno nilidhani yanatumika kwa watu nisio wajua tu kumbe hata watu ninao wajua na ambao tena wapo kwenye jamii nyonge ya watu wenye ulemavu. Watu wenye ulemavu sasa wamefikia Milion 4, jamii hii bado imeendelea kukumbwa na umaskini mkubwa unao sababishwa na ugumu wa mazingira wanayokutana nayo katika kutafuta maisha bora. Watu wenye ulemavu wamelia sana kuhusu changamoti zao lakini sauti zao bado hazisikiki katika vyombo vya maamuzi na mipango ya nchi, hii inatokana na uchache wa watu wenye ulemavu waliopata fursa kushindwa kutumia fursa zao katika kutetea na kushawishi vyombo vya maamuzi na vyombo vinavyotunga sera, sheria na mipango kukumbuka uwepo wa wa watu wenye ulemavu ili kusaidia utekelezaji wa sera na sheria zinazo toa fursa kwa watu wenye ulemavu. Ukweli ni kwamba ni walemavu wachache sana walioweza kupata fursa za uchumi, fursa za siasa na hata fursa za kijamii, Lakini hawa wenzetu wengi wamekuwa mabalozi wasiojali maslahi ya kundi hili na hata kufikia kujiondoa kiroho katika kundi hili ingawa ki mwili bado wana hesabika ni watu wenye ulemavu.fb_img_1480102785902

Kwa bahati mbaya jamii imetumia ulemavu wetu kama alama ya utambulisho (public figure) kiasi kwamba jamii inakutambua kwa ulemavu wako na si vingine kisha sifa zingine zinafuata na mara nyingi sifa mbaya za watu wenye ulemavu zimekuwa zikivuma kuliko sifa nzuri za jamii hii. Hili ni tatizo linalozaa utengano kwa jamii ya watu wenye ulemavu maana hawa wanaopata fursa kwa mgongo wa kundi hili wamejisahau na kujikuta wanapigania maslahi yao na matumbo yao bila kujali uwepo wa jamii ambayo imesababisha wao kupata fursa. Wenzetu badala ya kutuunganisha katika fursa, wao wameendelea kula dili na wasio husika. Badala ya kupaza sauti ya ushawishi na utetezi, wao wameendelea kukaa kimya na kuridhika kwa vinono wanavyopata. Badala ya kuanzisha miradi ya kuwezesha jamii hii wao wana anzisha miradi ya kitapeli katika jamii, wameshindwa kushawishi utekelezaji wa sera za walemavu ingawaje kila siku wapo angani kwenda mataifa ya wenzetu waliopiga hatua juu ya utekelezaji wa sheria na sera za watu wenye ulemavu, Wameshindwa kushawishi kuanzishwa kwa jumuiya ya walemavu katika vyama vyao vya siasa ingawa wao wamepata fursa kupitia jumuiya ya wanawake, wameshindwa kushawishi utekelezaji wa sheria no.9 ingawaje wamepewa utawala katika sheria na wizara ndani ya ofisi ya waziri mkuu, wamegeuza dhamana kuwa msaada, wamegeuza msaada kuwa mtaji na wametumia mtaji wa unyonge wa walemavu kuwa fursa kwao na familia zao

Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)
Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)

#Mytake
Wewe uliyepata fursa za uchumi, siasa na utawala kupitia walemavu, jiulize, Umeifanyia nini kundi hili linaloteseka na kunyanyasika kila siku wakati linakutegemea wewe kushawishi na kutetea mabadiliko yao? Ujue Mungu anakuona vizuri sana. Usijisahau ukadhani unaishi bila ulemavu na hata ukaukataa kwa maneno na matendo, bado utaendelea kuwa kwenye kundi hili maana hakunaga uponyaji kwa uumbaji wa Mungu labda kwa usanii na maigizo.fb_img_1480102909327

UKIMYA WA HAWA NDUGU ZETU UNAUMIZA NA KUKERA KULIKO HATA KELELE ZA WAPINZANI WETU. Badilikeni..

Asanteni

**Baadhi ya maoni ya watu**screenshot_2016-11-25-13-40-52-1-1 screenshot_2016-11-25-13-40-33-1 screenshot_2016-11-25-13-41-16-1

“HIVI KWELI HILI NDILO OMBI LA WATU WENYE ULEMAVU KWA MH. JPM?” ~~~~ Peter Sarungi

HIVI KWELI HILI NDILO OMBI LA WATU WENYE ULEMAVU KWA MH. JPM?fb_img_1479740222055Jana ilikuwa siku muhimu sana kwa makundi mbalimbali ya kijamii kama wakulima, wafanyakzi, watoto, wanasiasa, wavuvi, wazee, vijana, wanawake, wafanyabiashara na makundi mengine yanayo endana na hayo. Mimi nilikuwa mmoja kati ya wengi waliokuwa na hamu ya kusikia neno kutoka kwa JPM linalohusu jamii yangu ya watu wenye ulemavu Tanzania.

Kwa bahati nzuri katika fani ya uandishi wa habari, tunaye mwandishi wa habari bora kabisa aliweza kupata tuzo mbalimbali za ndani na nje ya nchi kutokana na makala na uandishi uliohusu maisha ya kila siku ya watu wenye ulemavu. Mwandishi huyo nguli anaitwa #Tuma_Dandi kutoka Chuo kikuu cha Dar es Salaam – Jounalism school. Hivyo moyo wangu ulikuwa umejiandaa kupata maswali/swali litakalo gusa changamoto kubwa kabisa za mtu mwenye ulemavu Tanzania. Tuna mshukuru sana Ndugu yetu #Tuma kwa utayari wake na kwa nia yake ya kusema maswala ya watu wenye ulemavu wakati wowote na kwa fursa yoyote.

Ninavyo amini mimi, kupata nafasi huru ya kumuuliza mkuu wa nchi swali ni nadra sana na ikitokea ukapata nafasi hiyo basi ni vizuri ukaitendea haki kwa kuuliza swali muhimu kwa jamii yako. Hivyo niliamini kuwa Mwandishi wetu Nguli angeuliza swali ambalo ni specific katika sector flan ambayo imekuwa na kero lakini kwa mshangao mkubwa, mwandishi wetu hakuuliza swali bali alitoa ombi juu ya utekelezwaji wa sera na sheria namba 10 ya watu wenye ulemavu. Maombi hayo yasiyokuwa na kero yalikuwa kama ushauri kwa Mkuu wa nchi ingawa naamini kuwa Mkuu wa nchi anaijua sheria hii na ndio maana akaweka wizara maalumu ya kishugulikia maswala ya watu wenye ulemavu. Kwa mtazamo wangu ule mkutano ulikuwa rasmi kwaajili ya wahariri kuhoji utekelezaji wa JPM kwa kipindi cha mwaka tangu achaguliwe kuwa mkuu wa nchi.

Mkuu wa nchi aliyapokea maombi hayo na kuelezea vizuri sana ni jinsi gani anavyo jali watu wenye ulemavu na hata kutaja viongozi wenye ulemavu alio wateua katika nydhfa mbalimbali ikiwemo nwibu waziri. Kwa majibu haya mazuri ya JPM ni dhairi kuwa kazi iliyobaki ni ya watendaji wake wakiongozwa na viongozi wenye ulemavu walio teuliwa. Wao ndio wana jukumu kubwa la kusukuma maendeleo ya kundi hii na hapo ndipo mwandishi wetu angeweza kupata maswali mengi ya utendaji yanayo gusa kero za watu wenye ulemavu kama vile ajira, elimu, uchumi, ujasiriamali, ushirikishwaji, afya na huduma zingine ambazo zimeendelea kuwa ngumu kwa kundi hili huku wizara yake ikiendelea kukaa kimya.

Kimsingi Mkuu alitaka kupima uwajibikaji wa wasaidizi na watendaji wake kwa mwaka mmoja kupitia maswali ambayo angeulizwa na yeye kutoa majibu.

Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)
Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)

#Mytake
Mh. JPM, jamii ya kundi hili hatukuwa na ombi hilo pekee lililoletwa na mwandishi wetu bali tulikuwa tunaka kuhoji kama ifuatavyo.

Tulipiga kelele sana iliyopelekea kuanzishwa kwa sheria namba 10 ya watu wenye ulemavu mwaka 2010 tukiamini kuwa sheria hiyo ndiyo mkombozi wetu, Ni miaka sita tangu sheria hiyo kuanzishwa bila utekelezaji, Je, serikali yako imefanya jitiada gani kwa kipindi cha mwaka mmoja kuhakikisha sheria hii inatekelezeka ki uhalisia? na je serikali yako ina mkakati gani ya mbele kuhakikisha sheria hii inendelea kutekelezwa?

Kwa swali hili naamini tungepata majibu ya JPM yenye kulenga utekelezaji uliofanyika na hata tungejua ni kipi kinenda kufanyika juu ya sheria hii, pamoja na hayo, swali lingewafumbua macho watendaji na wasimamizi wa wizara husika kuhakikisha wanaendelea kutilia mkazo utekelezaji wa sheria hii.

Asanteni sana
0713037798

“Tuamini lipi kati ya haya?” – Peter Sarungi

TUAMINI LIPI KATI YA HAYA?

Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)
Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)

1. Report za BOT zinaonesha kuna mdororo mkubwa wa uchumi wa nchi. hali inayopelekea vichochezi vingi vya uchumi wa nchi kuanguka kama vile utalii, taasisi za fedha, sector ya usafirishaji na uchukuzi, sector ya viwanda na kilimo.

2. Wanasiasa na viongozi wetu wanapinga kudorora kwa uchumi wa nchi wakituaminisha kuwa fedha zipo ila ni lazima ufanye KAZI. Wanasema eti wale wanao lia njaa ni wapiga dili waliokosa dili za pesa chafu.

3. Mtaani haijulikani nani ni msafi au mchafu, nani ana fanya kazi au mfanya biashara, nani ni mtumishi wa umaa au wa sector binafsi ila wengi wao kama sio wote wanalia njaa ya kuadimika kwa fedha mtaani.

Sasa sisi ambao tupo tupo tu tuamini lipi?

“Uchaguzi wetu Bongo Lowassa ndiye alitakiwa kuwa Trump? Are you serious or just kidding?”- Lemutuz

screenshot_2016-11-11-08-39-38-1 screenshot_2016-11-11-08-40-05-1 screenshot_2016-11-11-08-40-25-1

NINA HOFU NA KELELE ZA WABUNGE WA CCM KULIKO WABUNGE WA UPINZANI- Peter Sarungi

Imezoeleka katika bunge letu tukufu kusikia kelele za lawama na za kukosoa mipango na utendaji wa serikali kutoka kwa wabunge wa kambi rasmi ya upinzani. Kelele hizo zimewahi kusikika na kuibua kashfa nyingi na kukosoa sera, sheria, mipango na hata utendaji mbovu na hata kusababisha maamuzi magumu ya kufukuzwa kwa baadhi ya viongozi na wengine kujiuzuru nadhifa zao kama ilivyokuwa kwa Mh. Edward N. Lowassa. Lakini pamoja na hayo kufanyika bado serikali ilifanikiwa kupita majaribu hayo yaliyokuwa na wakati mgumu. Serikali iliweza kufanikiwa siku zote kupitia umoja na wingi wa viti vya wabunge walivyokuwa navyo bungeni maana waliweza kufunika kombe ili mwanaharamu apite. Hoja nyingi za wapinzani zilifunikwa kwa kura nyingi zilizokuwa zina maslahi ya kificha aibu ya chama na serikali.

Katika Bunge la kipindi hichi, mambo yamekuwa tofauti sana hasa katika kupiga kelele. Kelele nyingi na zenye uzito zimepigwa na wabunge wa CCM na zimepata Kick kuliko hata kelele za Upinzani. Ukiangalia wabunge waliokuwa vinara wa kutetea serikali wamefika mahala wamegeuka na kupiga kelele.

Maeneno mengi ambayo yamepigiwa kelele ni kama yamewakera wengi mpaka yameshindwa kuvumilika. maeneo kama uchumi, afya, demokrasia na utawala bora. Kelele hizi zinawwza kusababisha mpasuko mkubwa ndani ya chama tawala na serikali inaweza kupata vikwazo vigumu katika kutekeleza wajibu wake.

Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)
Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)

#Myatake
1. kuna uwezekano kuwa wabunge wanabanwa na wanachi wao na hata wao kupata wakati mgumu kuliko kipindi kingine, hivyo hasira zikawarudia serikali. 

2. Yewezekana wabunge wa CCM hawasikilizwi katika mapendekezo na ushauri wanao toa kwa serikali ama serikali haitoi ushirikiano kwa wabunge wake 

kuna msemo unasema kuwa adui mkubwa ni yule anayepatikana nyumbani kwako kuliko anayepatikana kwa jirani, Kuna haja ya serikali kujitathimini ili kulinda maslahi ya kutawala nchi lasivyo Jahazi litasumbuliwa na abiria wenyewe.

Asanteni sana
0713037798

“Wazee wa Kimarekani wanaomaliza generation yao now hawakuwa tayari kuona “dhambi” ya kumchagua Rais mwanamke inaangukia mikononi mwao”- Lemutuz

screenshot_2016-11-09-12-14-25-1screenshot_2016-11-09-12-15-06-1