Category Archives: General education

KUNA GHARAMA KUTETEA UKWELI – NAPE!

KUNA GHARAMA KUTETEA UKWELI – NAPE

Peter Sarungi (The next time)

Nimesikitishwa sana na taarifa kutoka ikulu, ingawa niliona ishara hiyo kutokana na mwenendo uliopo. Pamoja na hayo Nampongeza sana Mh. Nape Nnauye kwa karata ya ushindi aliyo cheza jana kwa maamuzi ya kutetea ukweli. Kwa karati hii, watanzania wamefuta Hasira, dhiaka na chuki walizokuwa nazo toka kipindi ulipo kuwa Msemaji wa propaganda za chama. Leo Umekuwa shujaa wa uhuru wa habari na naamini hivi vyombo vya habari vitakutunuku kwa maneno na matendo kwa kutetea ukweli. Nakutakia safari njema ya siasa, ukiweza basi anzisheni chama chenu wanasiasa wote mnao tengwa na chama kwa kuwa tofauti na mkuu maana sioni chama mbadala kitakocho wapa uhuru wa kufanya siasa zenu.

“Much of this success was built on my own hard work” -Monica Joseph

UKIPINGWA NA MKUU, VIZURI UKAJIWAJIBISHA. -Peter Sarungi

UKIPINGWA NA MKUU, VIZURI UKAJIWAJIBISHA!

Peter Sarungi (The next Speaker)

Ingawa ni vigumu kupata tamaduni za kuwajibika kwa viongozi wengi wa Afrika lakini bado kuna kila ulazima wa kuwakumbusha viongozi wetu na hata kuwafunza vijana ambao ni kizazi kinachochukua dhamana kutoka kwa wazee wetu juu ya umuhimu na faida za kuwajibika mwenyewe bila kushurutishwa.

Watanzania tunafunzwa na viongozi wetu kuwa na tabia za ajabu sana unapopata madaraka, tabia kama za ubabe, majivuno, dharau, ung’ang’anizi, ufisadi, uzembe na zingine nyingi ambazo tumekuwa tukizishuhudia kutoka kwa viongozi wetu. Tamko alilotoa Waziri wa Sheria la kupiga STOP ufungaji wa ndoa bila cheti cha kuzaliwa kuanzia mwezi wa tano na baada ya muda mfupi Mkuu wa kaya akatoa katazo la utekelezaji wa agilo la waziri wake. 

Kwa tafakuri ndogo, inaonesha kwamba agizo hilo la waziri halikupata utafiti wa kutosha na pia halukupita kwenye vyombo vya ushauri kama Baraza la mawaziri. Pia inaonekana agizo hilo limemkera sana Mkuu wa kaya kiasi kwamba akalitolea tamko yeye mwenyewe bila kutumia wasaidizi wake kama vile waziri aliye husika kutoa agizo hilo.

Kwa maamuzi aliyoyafanya Mkuu wa nchi kwa Waziri husika lina fundisho kubwa sana na angalizo kwa waziri husika. Ningekuwa mimi ni waziri husika ninge jiwajibisha kwa kushindwa kufikia viwango vya mkuu wangu wa kazi, maana inawezekana akanitumbua ama akanisahau kwenye marekebisho ya baraza la mawaziri.

Nafikiri ni muda mzuri kwa Waziri Mwakiyembe kuji pumzisha ikiwa ni hatua ya kujiwajibisha ili aendelee kubaki na heshima yake iliyo tukuka kwa nchi. Kuna faida kubwa ya kujiwajibisha mwenyewe kuliko kusubiri kuwajibishwa tena kwa aibu, nasema hayo kwa sababu na mimi mpaka leo naendelea kunufaika na hii tabia ya kujiwajibisha ambayo nimewahi kuifanya sehemu mbalimbali za uongozi wangu.

By the way kuna kazi sana kutoa tonge kutoka kwenye midomo ya waafrika, wapo tayari kunyang’anywa kwa nguvu kuliko kulitema wenyewe hata kama tonge ni chungu.

Asanteni.

“NIMECHAGUA UKWELI KWENYE SIASA, SIO BARIDI WALA MOTO.” -Peter Sarungi

Peter Sarungi (The next Speaker)

Siasa safi zinahitaji kuwa na demokrasia ndani yake, kuwe na uhuru wa kutoa mawazo mbadala, kuwe na desturi ya kuvumiliana hasa pale mnapopingana mawazo na kuwe na tabia ya kutafuta na kusema ukweli hata kama ukweli huo utakuwa mchungu.

Mtindo wa vijana wengi wa sasa ni wa ajabu sana katika siasa. Mtindo ulio gubikwa na tabia za uongo, unafiki, fitina, wasaliti, ndumilakuwili, kujipendekeza, kutafuta sifa, kukurupuka, ushabiki, na unazi usiokuwa na tija kwa taifa. Tabia kama hizi zina fifisha ubunifu, uzalendo, umakini, ujasiri na umahiri kwa vijana katika uongozi na uwajibikaji.  Tumejenga jamii ya vijana walio gawanyika kihisia, itikadi, maneno na kwa matendo yao, waoga wa kutetea ukweli, wepesi wa kushindwa na uovu, walio tayari kusema vya kukaririshwa. Ndio maana kuna vijana walio tayari kukosoa jambo lolote kutoka upande wa pili hata kama ni jambo jema kwa taifa na wapo tayari kusifia jambo lolote la upande wao hata kama ni sumu kwa Taifa. Wameamua kuwa baridi ama moto.

Mimi nimekataa kuwa sehemu yao, kuwa mtumwa wa fikra zao, kutumika katika malengo yao. Nimeamua kuwa mfuasi wa ukweli na kwa fikra huru. Nahitaji Ukweli ili uniweke Huru, ukweli utakao tibu Taifa ili vizazi vijavyo vipate kufaidika na ukweli huu.

Unga kuchagua ukweli ili tujenge Taifa lenye kuheshimu ukweli.

Asanteni sana.

KIIZA TUNDU LISU BASIGYE KOROKONI- Peter Sarungi

Peter Sarungi (The next Speaker)Ipo siku masikio yata ona badala ya kusikia na macho yatasikia badala ya kuona. Wakati ambapo utatamani ujifiche chini ya milima lakini haitawezekana, wakati ambao wanawake wengi wataomba kuitwa kwa jina la mwanaume mmoja huku wakijilisha na kujivisha wenyewe.

Kwa sasa namfananisha Tundu Lisu na mwanasiasa mkongwe wa vikwazo kutoka kwa jirani zetu Uganda Mh. Kiiza Besigye. Kwa hivi vikwazo vya kuwekwa korokoroni na kupewa kesi nyingi za uchochezi kwa Mh. Tundu Lissu huku akiendelea kuwa jarisi na mwenye kutetea ukweli na hata kutenda na kuheshimu sheria. Sasa ninaona umuhimi wa Tundu Lisu kuwa Raisi wa TLS maana kwa sasa tunahitaji viongozi wanao hoji mifumo kandamizi bila uoga ili kulinda maslahi ya Taifa na watu wake. Kwa courage aliyonayo Mh. Tundu Lissu katika siasa za kweli, naamini hichi ni kipindi cha watu kama akina Lissu kunyanyuka na kuungwa mkono kwa makusudi.

Ningekuwa ni mwanasheria, ningemchagua Lissu kuwa Raisi wa TLS. By the way hiyo TLS na majukumu yake nimeifahamu kipindi hiki kupitia Lissu na inawezekana sio mimi tu, tupo wengi.

Asante Lissu, Go go go go Lissu

TAFAKURI YA LEO JUU YA WABUNGE WA CCM.- Peter Sarungi

Peter Sarungi (The next Speaker)

Tabia ya wana siasa kabla ya kuwa watawala ni kama tabia za wachumba ambao bado hawajafunga ndoa. Tabia yao kuu ni kuhaidiana mazuri, kusifiana, kuelekezana kwa lugha ya kuvutia, kutiana moyo, kuoneshaana upendo wa agape lakini pia kuna tabia moja mbaya ya walioyo nayo ya kuficha udhaifu wao na mabaya yao.

Kila inapoitwa leo, napata fursa ya kujua tabia za mkuu wa nchi kupitia kauli zake na matendo yake. Niliwahi kukiri hapo mwanzo kwa kusema kuwa Mkuu wa kaya anasimamia vizuri kauli na matendo yake wakati wa kampeni nikidhani ataendelea kutawala kupitia kauli zake za kusisitiza umoja wa nchi. Nahisi ni mihemuko ya muda iliyo niathiri.

Pamoja na changamoto hizo bado maisha na siasa zitaendelea na ni lazima tuendelee kuwaoma wabunge hasa wa CCM ambao ni 75% kusimamia kwa kuikosoa, kuisema na hata kuipongeza serikali wanapo kuwa bungeni maana hiyo ndiyo kazi tuliyo watuma. Pamoja na mtikisiko huu ulio wapata wabunge kutoka kwa Mkuu wa kaya kama ilivyo ripotiwa na gazeti la mwananchi bado mtaendelea kuwa wabunge mlio pewa dhamana na wananchi ya kuwa wakilisha bungeni katika kuisimamia serikali.

Tusijenge Taifa la chuki na uadui unao tokana na siasa, tuki ruhusu hilo basi hatutokuwa salama maana ukweli ni kwamba chuki na uadui havina mipaka, nikikuchukia kwenye siasa usidhani nitakupenda uraiani. Hiyo ni mbegu mbaya itakayo tafuna jamii yetu.

Tujitahidi kujenga jamii ya kuvumiliana, kushauriana, inayo heshimu fikra tofauti na inayoweza kuwa karibu hata kama watakubali kutokukubaliana.

Mungu tubariki huko tuendako.

TAFAKURI YA LEO JUU YA CCM MPYA -Peter Sarungi

Peter Sarungi (The next Speaker)

Nimepata taarifa juu ya kuzaliwa CCM mpya iliyo badilika katika muundo wa chama na uendeshaji lakini ikiendelea kubaki na itikadi yake ya zamani. CCM Mpya iliyosemwa na mwenyekiti wake kwamba itakuwa chama kwa wanachama yaani chama kitakacho milikiwa na wanachama wenyewe tofauti na mwanzo. Inasemekana kabla ya upya huu, chama kilikuwa kina endeshwa na wanachama wenye nguvu za fedha, vyeo na hata umaarufu. Sasa kwa upya huu, chama kitaendeshwa hata na mlalahoi bila kujali umaarufu wake, cheo chake ama fedha zake… (SAFIII SANAAA..) 

LAKINI..????? Tafakuri yangu ni jinsi gani chama hiki kitaendeshwa na kumilikiwa na wanachama kama inavyoitwa CCM Mpya… ………Ikiwa kiwango cha uwakilishi wa wanachama hawa kwa idadi katika vikao muhimu na vinavyo toa maamuzi muhimu ya chama umepunguzwa kwa zaidi ya nusu??? Yaani kutoka mia tatu na kitu hadi mia moja na kitu..!!!Ikiwa idadi ya vikao vilivyokuwa viki tathmini utendaji wa chama na serikali vimepunguzwa???Chama chenye wanachama na wapenzi wapatao milion 8, kutoka mikoa 35, ikiwa na jumuiya mbalimbali karibia tano na matawi lukuki, chama kinacho ongoza nchi kuongozwa na wajumbe 165 badala ya 385 alafu tuna sema CCM mpya ya kumilikiwa na wanachama??

Hili panga ni kali na sijui kama hawa vijana wenzangu Benard R. Shigela ?na Yesaya Shamsele ?walio anza vizuri kujifunza siasa na uongozi kama watapata nafasi na fursa ya kuwepo kwenye vikao vya CCM mpyaJJk alidokeza sababu ya mabadiliko haya kuwa ni UKATA…. Tunasoma Namba.. Hii sababu ya kuifanya CCM kumilikiwa na wanachama bado kwangu haija ingia akilini labda wadau watufafanulie..

Dr. Magufuri and the agricultural policy…….?!!! -Chege Kalahala

Is he a firm proponent of a free market economy or he simply “dont get it” with regard to the economics behind the agricultural industry???

Or are we witnessing the absence of “coherent and consistent” agricultural policy?

Magufuri told farmers that, the govt will not provide assistance in case of food shortage…..the implication is that, it will be farmers’ fault that there will be food shortage…….mhhh!!

Overall, this just says one thing; either there is no such a thing as an agricultural policy or it is not well developed to reflect some unforessen contingents like bad weather.

European have Common Agricultural Policy(CAP); that have emerged from its birth in the 60s. The aim is simply this; to help farmers in case there is a need for that. The philosophy behind the policy is that, unprotecting the industry will lead to food shortage. What else? Prices fluctuations caused by alternating good and bad season is not a welcome for a smooth economic growth of any country. To stabilize agricultural products prices, and ensure a good standard of living for its citizens, countries enact these kind of policies. 

USA has what it calls Agricultural Adjustments Act; with the same goal. The policy has evolved from its inception in the 1930s.

Tanzania should not second-guess itself when it comes to the agricultural sector. The industry needs govt protection. Magufuri’s statements were so unfortunate.

If more diverse economies; less-dependent on agriculture as the engine of their economic growth like EU and USA have the policy in place,…..why not Tanzania?!!!

CCM WANA HAKI YA KUFUKUZA WASALITI. -Peter Sarungi

Peter Sarungi (The next Speaker)

Huwa sipendi kuingilia siasa za ndani za vyama  vingine lakini huwa inanilazimu kwa sababu chama kama cha ccm kinatawala serikali hivyo maamuzi yake yana athari kwa uendeshaji wa serikali na Taifa kwa ujumla.

Nimeona mjadala wa wafuasi wengi wa upinzani wakilalamika juu ya maamuzi ya fukuza fukuza ya wanachama wa ccm wanao itwa wasaliti. Wanapinga na kulaani maamuzi halali yaliyotewa kutokana na vikao halali.

Mimi naunga mkono maamuzi hayo maana watu walio fukuzwa wamepatwa na mazingira ya kusaliti chama. Ni kama Mh. Zitto alivyo vuliwa uana chama wa Chadema Tanzania kwa tuhuma za usaliti ulio elezewa na viongozi wa kushirikiana na chama tawala. Walio fukuzwa wana mazingira ya kusaport harakati za Lowasa Edward kushika dola kupitia vyama vya upinzani wakati wao wakiwa na vyeo katika chama cha ccm, huu ni usaliti usio takiwa kufumbiwa macho. 

Fukuza, fukuza, fukuza hadi wale wote karibia 75% ya wajumbe wa almashauri kuu ya NEC walio imba wimbo wa kuwa na imani na Lowasa wafutike katika vyeo vyao ndani ya ccm, mkìweza wafukuzeni na wabunge ambao bado ni waumini wa Lowasa.

Mkiamua kujenga safu ya mwenyekiti wenu kwa mgongo wa kusafisha chama, nawashauri mfanye kwa uhakika na asibaki hata mmoja aneyeweza kuhoji na hata kusema tofauti na mkuu. Hilo ni jambo lenu la ndani na wala sisi tusio wanachama hatupaswi kuingilia na ndio maana nina pinga kwa nguvu zote wanao laani na kubeza maamuzi haya.

Nawatakia mkutano mwema katika kujenga ccm mpya na kuiacha ccm ya Nyerere, ccm ya mwinyi, ccm ya mkapa na hata ccm ya Jk.

Poor Makonda…! by Chege Kalahala

Chege Kilahala

In politics, don’t ever let your opponents have a chance “to define” you before you have defined yourself. Thats why politicians in the western world like to write books about their life stories. It gives them a chance to “set the records straight” before their political opponents hijack their stories and paint them however they see fit.

Considering his background, Makonda should have dealt with his past a while ago……! And he still can……..

Mh. Paul Makonda

He has a personal story to tell….of a guy who…despite many obstacles….swam against the tide to reach where he is…..a story that can resonate with a lot of aspiring young men and women…..from all those failures in school and yet be able to pick up yourself and get going…..thats inspiring….! Of course, he will have to start by admitting his blunder and failure to be honest with Tanzanians upfront……My wish is that, there were good PR (public relations) experts in Tanzania….

Well….what can we do?!

“SI KWAMBA NI MCHAPA KAZI TU BALI PIA NI MZURI WA MUONEKANO” Mkuu wa kaya

Peter Sarungi (The next Speaker)

 Moja ya sifa ya Mkuu wa kaya katika hotuba zake ni kupenda kutoa mifano ama utani yenye chembechembe za ukweli. Sifa kama hizi akipewa mama, mke, dada au hata bibi inaleta furaha na inajenga kujiamini kwao.

Nitumie fursa hii kumpongeza Mama Salma Kikwete (Malkia wa nguvu wa Taifa) kwa kuteuliwa kuwa mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Naamini sifa ulizo pewa na Mkuu zita akisi uwezo wako wa kutetea maslahi ya Taifa na wananchi wake.

Nafasi uliyopata sasa inakusogeza karibu zaidi na matatizo ya wana wa nchi lakini pia inakupa uwezo zaidi ya kuleta suluhisho ya matatizo hayo tofauti na ulivyokuwa First Lady. First Lady ni ceremonie title, ulikuwepo kwaajili ya kupamba kazi ya baba, kumshauri na kusapoti kazi zake kupitia WAMA. Uwezo wako binafsi ulifichwa ndani ya mafanikio na sifa za baba. Sasa ni zamu yako kuonesha ushujaa wako kwa nchi na hasa kwa wale wanao beza uteuzi huu, onyesha umuhimu wa fursa kwa wamama kama alivyo onesha Mama Hilary Clinton.

Nakutakia Kazi njema na utendaji mzuri katika kutumikia wananchi wa tanzania kupitia Bunge. Mama usiogope kukemea na kusema ukweli. Ni Haki yako kusema ukweli hata kama utabaki peke yako, bado ukweli huo ulio usema utaishi zaidi yako.

Asanteni.

HIZI KESI ZINA DHOOFISHA SANA UPINZANI- Peter Sarungi

Kuna msemo unasema “Adui mwombee njaa, atainua mikono juu hata kama ni Shujaa”

Msemo huu unatukumbusha kwamba siku zote binadamu umuombea mabaya mpinzani wake, ndivyo tulivyo umbwa na hata katika siasa ndivyo ilivyo tena ni zaidi ya kuomba mabaya na kutenda mabaya kwa mpinzani wake.

Upinzani una kabiliwa na kesi nyingi sana katika mahakama zetu. Kesi hizi zipo kwa viongozi kuanzia ngazi ya ya mwenyekiti Taifa hadi kwa wenyeviti wa vijiji mikoani. Uwepo wa kesi hizi zina athiri upinzani kwa njia tatu.

1. Ki Uchumi: Uendeshaji wa kesi una gharama kubwa mno na kwa nchi zilizoendelea, kesi ni njia moja wapo ya kufilisi au kupunguza uchumi wa mtu ama kampuni. Mfano: Mike Tyson pamoja na mambo mengine ali filisika baada ya kugharamia kesi yake ya kubaka.

2. Ki Siasa: Baada ya uendeshaji wa kesi, kinacho fuata ni hukumu. Hukumu yaweza kuwa nzuri ama mbaya kwa upinzani, inapokuwa mbaya inaleta pengo kubwa la kisiasa kwa upinzani. Mfano: Mh. Peter Lijualikali (MB Kilombero) anatumikia hukumu ya kifungo cha miezi sita jela. Hukumu hii ina dhoofisha nguvu ya siasa na hata kuleta pengo la utendaji wa mwanasiasa huyu kwa walio mchagua.

3. Ki Jamii: Inapotokea kiongozi wa kisiasa anapatwa na tuhuma, anashitakiwa na kuhukumiwa basi wanao umia kisaikolojia ni jamii yenye imani kubwa na kiongozi huyo. Mfamo Mh. Mbowe (MB Hai, KUB na M/kiti Chadema) anapopatwa na tuhuma ya kukwepa kulipa kodi au kujihusisha na Dawa, wanao umia zaidi kisaikolojia ni wakereketwa, wapenzi, mashabiki, wananachama na viongozi wa Upinzani walio chini yake.

Hizo njia tatu kwa pamoja zinaleta athari za kudhoofika kwa wanasiasa mahiri na machachari wa upinzani

#Kumbuka Dhamani sio ushindi, Tunaye kaimu judge mkuu kwa mhimili huu, Kuna wanasiasa walio nyamaza baada ya kesi. Pole G. Lema (MB Arusha) na wananchi wa Arusha kwa mateso ya kisaikolojia mliyo yapata kwa muda wote.

“It is morally wrong to punish them for their efforts to better themselves; regardless of how they seek to better their lives”-Chege Kilahala

Nakumbuka enzi za Nyerere……wakati alipokuwa anakamata vijana wasio na kazi kwa kosa la “uzururaji”…..kwangu mimi naona kazi ya serikali ni kuweka sera za kuinua uchumi na kuongeza kazi (to create economic policies that will create opportunities for young people)…….kukamata vijana ambao wanatafuta riziki wakati serikali yako imeshindwa kuinua maisha yao kwa kuweka uchumi bora ni “morally wrong”. Na nalaumu hiyo sera ya Nyerere wakati ule. Nyerere was supposed to own his failure; failure to enact laws that will create policies for economic opportunities for young people.

Likewise, while I don’t support impersonation and forgery, I think we should be considerate of people who seeks second chances in life…..using other people’s certificates to advance their career opportunities etc etc

Who is to blame for that? Again; the government and its education policies. For not enacting laws that will give second chances to these kind of people. In most developed countries, you can opt for other educational alternatives that are equivalent to the education level you seek.

The govt needs to work harder to create an environment in which people who failed in their exams, young girls who caught pregnancies while at school and other who dropped out of school for any reason, can do “a comeback” later in life. Lack of opportunities and alternatives makes these people turn to forgery and impersonation.

It is “morally wrong” to punish them for their efforts to better themselves; regardless of how they seek to better their lives (except if its killing or stealing).

Kulipwa kwa kazi ya campaign ya chama ni halali yako!- Alpha Igogo

Alpha Igogo
Blogger

Katika kila jambo au shughuli yoyote lazima kuna fedha zitatumika tu! Hii haijalishi ni shughuli ya chama, kanisa, msikiti, kijamii, au za kipagani lazima fedha zitahusika! Lakini sasa uingizaji na utoaji wa hizo fedha zinaweza kuwa katika mfumo uliyo rasmi (yani kuna kuwa na budget, mfumo wa malipo, na washuhudiaji) au siyo rasmi (yani hakuna accountability ya aina yoyote ile).

Tukirudi katika mada yetu kama kichwa cha habari kisemavyo, kuwa, “kulipwa kwa kazi ya campaign ya chama ni halali yako” basi ngoja tuzungumzie hilo kwa sasa. Kampeni za siasa huwa lazima chama kinajipanga kwa mikakati (strategies) ya jinsi ya kufanya campaign yenye mafanikio. Na moja ya mikakati hiyo ni jinsi ya kukusanya pesa rasmi kwaajili ya kukamilisha mikakati hiyo! Hapo ndipo utasikia kitu ‘budget ya campaign’. Pia kwa serikali ya Tanzania huwa wanakitu kinaitwa posho / ruzuku ya chama wakati wa campaign!

Hiyo budget ya campaign haitumiki tu kununulia vitendea kazi vya campaign bali pia kuwalipa wanachama / makada watakao kuwa teyari kufanya campaign hiyo kulingana na malengo ya chama chao. Ndio maana wakati wa campaign huwa wana aajiriwa watu maalum wa kufanya campaign au kikosi maalum cha nguvu kazi kwa ajili ya campaign husika kwa mfano anaweza ajiriwa Campaign Manager, au Financial Controler kwa ajili hiyo tu!

Sasa wewe kama ni mwanachama uwe mtu wa kawaida au “celebrity” kupewa fedha kwa ajili ya campaign ni kitu cha kawaida, ni swala ambalo linatambulika kisheria, na zaidi ya yote ni halali yako!

Wewe unapo acha shughuli zako za uzalishaji wa kila siku nakwenda kufanyia chama campaign nilazima chama kikupe hela za kujikimu maana utahitaji hela ya kukutoa point A to Z, utahitaji kula, utahitaji kulala kama ni nje ya mahala unapo ishi! Huwezi kuchukua pesa zako binafsi kufanyia chama campaign wakati kwanza umeacha shughuli zako za uzalishaji, pili kama una familia inamaana budget ya familia utaivuruga kwa mambo ya campaign.

Jamani, hata makanisani kuna budget ya kutembelea washiriki ambao ni wagonjwa, wajane n.k nawatu huwa wanapewa pesa za kujikimu na safari kama hizo. Hivyo si ajabu mtu kulipwa kwa shughuli ya campaign kwani hizo ndizo zile hela wenyeviti na viongozi wengine wa chama wanatumia kwa matumizi yao binafsi haswa kama hakuna mwanachama au wanachama ambao wanaweza ku-question uongozi! Kiwango / kiasi cha ulipwaji waweza tofautiana kutokana na nguvu aliyo nayo mtu huyo pamoja na makubaliano yao. Fedha zote zinazo ingia kwenye budget ya campaign ya chama lazima ziwe kwenye mfumo rasmi unao eleweka! 

Labda kama baba yako ni Mzee wa “Vijisenti” (you don’t need that kind of “petty” money)  kama sivyo kulipwa kwa kazi ya campaign ya chama ni halali yako!

Mungu ibariki Africa. Mungu ibariki Tanzania.

 

 

HATA SAULI ALIKUJA KUITWA PAUL! -Peter Sarungi

HATA SAULI ALIKUJA KUITWA PAUL Injili ya Yesu kristu inaeleza kuwepo kwa Sauli aliyebadilika na kuitwa Paulo. Injili inamwelezea Sauli kama kiongozi wa kijeshi aliyekuwa ni katili kupita kiasi, asiyekuwa na huruma, aliye chukia, kuwatesa na kuwa hukumu kifo wana wa Mungu. Lakini pamoja na machukizo haya yote mbele za Mungu bado Mungu alikuwa na mpango mzuri naye.

Mpango wa Mungu ulikuja kutimia na Sauli akaitwa Paulo. Kupitia jina la Paulo, tabia zake zilibadilika na akawa mtumishi wa Mungu aliyeweza kuhubiri injili na kuandika vitabu vingi vya injili kuliko wanafunzi wote wa Yesu kristu alio wachagua na kuwapa kazi ya kueneza injili. 

Hivyo sishangai kama Daudi akikimbia jina lake na kuitwa Poulo, maana yawezekana kwa jina la Daudi alikuwa mnyonge, kilaza, mvivu, mwoga, aliyefeli kwa kupata fa fa fa zote katika matokeo ya fom 4. Lakini kwa kuitwa Paulo emebadilika na kuwa jasiri, mchapa kazi, kiongozi mbunifu na mwenye kuthubutu, aliye faulu hadi chuo kikuu, aliyetenda makubwa katika uongozi wake kuliko hao wateule wa Mkuu. 

#MyTake 

Na Peter Sarungi (The next Speaker)

Kuna majina mengine yana Nuksi, hayaendani na ndoto zako na wala hayakusaidiiii. Unaweza ukawa una lalamika kushindwa kila jambo jema unalo jaribu kwa nguvu zote huku ukimshirikisha Mungu wako bila mafanikio kumbe ume sahahu kwamba jina lako halijabeba future unayotaka. Tuchunguze majina yetu hasa haya ya Ulaya.

Mwanangu Fidele siku akiona jina lake halimsaidii kufikia ndoto zake nitamruhusu na kumsaidia kubadili jina ???? Joks..

Lemutuz:- Mjadala wa vyeti hauna tija!

UKIWA MDHAMBI USIHUKUMU WADHAMBI- Peter Sarungi

UKIWA MDHAMBI USIHUKUMU WADHAMBI. 

Na Peter Sarungi (The next Speaker)

Niliwahi kusema kwamba vita alivyo chagua Makonda ni vita vinavyo hatarisha ustawi wa maisha yake. Mpaka sasa Mh. Makonda anapigana vita nne kwa yeye kuanzisha vita moja ya madawa.

1. Vita juu ya uhalali wa mali zake

2. Vita juu ya uhalali wa Elimu yake

3. Vita vya kisheria dhidi yake mahakamani

4. Vita dhidi ya Bunge na maazimio yake Maandiko matakatifu yanaeleza jinsi Yesu kristu alivyotoa kauli kwa wayahudi waliotaka kumwadhibu mwanamke aliye fumaniwa akizini kwa kutumia sheria za Musa……Alisema, “Kama kuna aliye msafi(asiye na dhambi) kati yenu basi na awe wa kwanza kumpiga mawe huyu mwanamke aliyefanya dhambi”

Hii ni kauli nzito sana kwa dunia ya sasa, Dunia inayotawaliwa na uwazi na kumbukumbu za kiteknologia, Dunia iliyo na macho pande zote, Dunia iliyojaa unafiki, usaliti, chuki, visasi, uongo, uzandiki, kashfa, fitina na machikizo mengi baina ya binadamu mmoja na mwingine.

Kwa Dunia kama hii… Ni vizuri tukaishi vizuri na jamii, tukaheshimu uongozi kam dhamana, tukajitakasa na dhambi kabla ya kuwatafuta na kuwahukumu wenye dhambi, tukajifunza kubakisha maneno ya kesho na keshokutwa.

Pole Mh. Makonda, ulianzisha vita moja lakini sasa unapigana vita nne tofauti.

Mungu akusaidie na akulindie roho yako isije ikapondeka kwa maneno na matendo ya binadamu wenzio…..Amina

2020 ni Pagumu!- Peter Sarungi

                    2020 NI PAGUMU!

Na Peter Sarungi (Next Speaker)

 Ikatokea Mungu akakubariki kufika 2020 ukiwa hai na mwenye afya nzuri basi utakumbana na changamoto ya joto kali la siasa ambalo halijawahi kutokea nchini. Kwa Lowasa Edward, 2020 ni mwaka wake wa mwisho kujaribu kufikia ndoto zake za kutawala nchi, ni kama ana bunduki iliyobaki na risasi moja ndani ya mapambano, hivyo ni lazima apambane kwa akili sana tena kimya kimya ili kutafuta target sahihi ya kufyatua risasi yake kwa adui. Ndio maana kwa sasa Lowassa anajipanga kimya kimya akiamini matokeo yake ni 2020.Kwa JPM, 2020 ni mwaka wake wa kuimarisha utawala wake na hasa kupata matokeo yatakayo leta taswira ya kupwaya kwa upinzani nchini. Hivyo kwa sasa anajipanga kwa matendo na kwa mifumo ndani ya chama na nje. Kutokana na nguvu alizopewa Raisi kupitia katiba ya nchi, ni kazi nyepesi sana kutengeneza mfumo utakao kusapoti mbele ya safari hivyo tutegemee mifumo hiyo kukamilika 2019.  

Kwa wananchi, 2020 ni mwaka wa majaribu sana kwao. Mpaka sasa bado wananchi wengi hawajui mwisho wa utawala huu ukoje, hawajui kama kutakuwa na mazuri ama mabaya ndani ya miaka hii mitatu iliyobaki (2017, 2018 na 2019) ikitokea uchumi wa mwananchi ukakua hadi kufika kipindi cha JK basi JPM atakuwa amepiga risasi ya ushindi kwa wananchi maana mpaka sasa amefaulu sehemu kubwa hasa ya ufisadi na nidhamu lakini amefeli kwenye UKATA wa wananchi, kuna malaika wameanza kuishi kama mashetani. 

Kuna Hash tag mbili zinazovuma mitandaoni

1# Nitamchagua tena 2020

2# Usirudie kosa 2020

 

Tafakari…. Chukua Hatua.

Kama unazifahamu tuambie!-Jackline Mengi

“Women are everywhere but Queens are scarce”!