Category Archives: Inspirational stories

“If you have to prove it means you really don’t have it. The grace of GOD doesn’t come with stress.”

If you have to prove it means you really don’t have it. The grace of GOD doesn’t come with stress. If you must go through stress to get attention means you are fooling yourself. When GOD makes you a star you will never struggle to shine. If you have it flaunt it, but if you don’t have it then stop living in pain. Fashion police is equal to mental slavery. Stop going through stress just to be in vogue you can never be faster than life. The antics of today were once upon in vogue. Wear what looks great on you, those who loves you will accept you for who you are. Stop spending the money you don’t have to oppress the people who don’t really matter in your life. Those who truly matter don’t care as long as you’re not walking naked on the street. The only way to cut your coat according to your size is to know your real size. BE HONEST WITH YOURSELF. There’s no point in wearing expensive designer shoes and then you start walking like SHREK painfully in debts. The greatest form of slavery is a mental slavery, to be prisoner in your ownn soul while the greatest follishness is to fool yourself, like the blind man who pretends to be sleeping by closing his eyes. Stop trying to fit in to the status you don’t belong, that’s why shoes come in diffrent sizes. Friendship is not a do die. If you must beg people to accept you for who you are means your self esteem is dead. A low self esteem can be cured but there’s never a remedy for a NO self esteem. If their class is too high CHANGE YOUR SCHOOL. Age has nothing to do brain. Growing up and growing old are never the same. Growing old is a mandatory while growing up is optional by choice. Until you fully learn and understand the art of standing alone, you may not have any stand in life. “~~~Akin Al Ameen®™2017

***picha za  Mengi’s family has nothing to do with the story. Nimezipenda tu***

“Don’t underestimate your dream”- Jackline Mengi

Btw, lile tangazo la Amorette is one of very few best Ads in Bongoland! Kudos to Jackline and your team!

Malkia wa nguvu 2017: Hongera sana Mwanaidi Mayowela, pongezi kwa Clouds TV!

Nilikuwa sijapata muda wa kuwapongeza washindi na waandaaji wa sherehe za “Malkia wa nguvu” hivyo naomba nichukue muda huu kuwapongeza!…………Kwakweli kama kuna kitu ambacho kimenivutia sana na kunigusa kwenye TV za Bongoland; basi ni hii sherehe ya Malkia wa nguvu. Sababu kuu yakunivutia nikuona kuwa waandaaji walichukua muda wao kufanya kazi ya kujua nani anastahili kupewa tuzo hiyo ambapo imekuwa tofauti sana na events /awards nyingi sana za “Wabongo” wengi kwani mara nyingi ni zakujuana juana. Yani authentication ya awards inakuwa haipo kabisa!!

Hongera sanaaaaaa Clouds TV mmenifanya niangalie hii event mara zote mlikuwa mkiirusha hewani! Natumaini na wengine wataiga mfano wenu. Pia hongera sana dada Mwanaidi Mayowela kwa kulitwaa taji kwani unastahili kwakweli! Ubarikiwe sanaaaaaa wewe na familia yako! Nawashindi wengine wote pia nanyi nawapongeza sana. Mungu azidi wabariki.

Malkia wa nguvu; Mchapa Kazi, Mbunifu,  Jasiri!

In loving memory of Ontlametse Phalatse

Ontlametse ni mtoto alikuwa ana ni-inspire sana! Nilikuwa namfatilia sana kwa Instagram, nilivutiwa sana na inspirational speech zake na jinsi wazazi wake walivyo mlea na kumjengea confidence kubwa sana ya kujikubali jinsi alivyo, kujiamini kuwa anaweza na anastahili kuishi kama wengine, na kujipenda! Nimeguswa sana na kifo chake, may her soul rest in peace! ……Ee Mungu naomba uniongezee ujasiri niweze ku-overcome all my fear and conquer them with greatness just like Ontlametse, Amen! 

HATA KWETU TUNAO MALKIA WA NGUVU.  HONGERA SANA MADAM SOPHEY MBEYELA. -Peter Sarungi

 

 Nikiwa kama mwanaharakati wa kutetea haki na kukuza utu wa watu wenye ulemavu, jukumu langu kubwa ni kukusogeza karibu na jamii hii ili sote tujue mazingira ya watu wenye ulemavu kwa kukuonesha changamoto na mafanikio yetu katika kuchangia maendeleo ya jamii. Tunaamini ushirikiano wako kwetu utaongezwa ikiwa utajua mazingira yetu.

Leo natumia jumapili hii kupongeza mafanikio aliyoyapata dada yangu Sophey Mbeyela baada ya kutwaa Tunzo ya Malkia wa Nguvu kwa mwaka 2017 kutoka Clouds Media kupitia kampeni yao ya kuwatafuta Malkia wa Nguvu kila mwaka. Anapenda aitwe Madam Sophey, ni moja kati ya akina dada shupavu, asiye kata tamaa na mwenye kufuata ndoto yake kutoka katika kundi la watu wenye ulemavu. Kazi yake kubwa ni mwalimu lakini pia ni mwamasijashi (Motivator) mzuri sana anaye warudisha vijana walio kata tamaa katika msitari, pia amekuwa akiamini katika kutoa na hivyo ameendelea kutoa misaada mbalimbali kwa jamii yenye mahitaji maalum kama vile watoto na watu wenye ulemavu hasa wanafunzi. Record yake ni nzuri sana kwa jamii yetu ya walemavu na amekuwa akichukua hatua mbalimbali katika kuhakikisha jamii inapata ustawi.

Nichukue fursa hii kumpongeza sana kwa mafanikio anayo endelea kuyapata na nimtie moyo kwa kusema HAKIKA  HIYO NDIO DUNIA YAKE ALIYOPEWA NA MUNGU, ASITAFUTE DUNIA NYINGINE..

Tafadhali kama unapendezwa na mafanikio haya kutoka katika jamii ya watu weye ulemavu basi andika chochote cha kumpa nguvu Madam azidi kutoa mchango kwa jamii.

“Much of this success was built on my own hard work” -Monica Joseph

“Ninafurahi kujumuika na akina mama na akina dada nyuma ya kampeni hii” -Jokate Mwegelo

“Wenye mioyo na fikra za upendo hubarikiwa zaidi”- Jackline Mengi

Ukichagua upendo kuendesha maisha yako utaishi kwa furaha na amani sana kwani utaonyesha upendo,utazungumza maneno yenye upendo,na utachagua upendo katika kila jambo,hata pale penye mchanganyiko wa chuki na upendo utachagua kuona upendo na kupuuza mengineyo.Siku zote wenye mioyo na fikra za upendo hubarikiwa zaidi na hiyo ndio siri ya maisha.

HAPPY WOMEN’S DAY 2017- Peter Sarungi

Peter Sarungi (The next Speaker)

 Nitumie siku hii ya leo kuwatakia heri wanawake wote duniani kwa mchango wao mkubwa na wa kutukuka katika kuendeleza dunia. 

Kipekee nimshukuru Mama yangu kipenzi Bi. Martina Sarungi kwa kuendelea kuwa mama bora kwa watoto wake. Nimtakie maisha marefu na yenye furaha na afya tele ili hata wajukuu na vitukuu waje wafaidike kwa busara na maombi yake.

Pia nimpongeze Mama fidel kwa kuchagua kuwa mama mwema na mwenye malezi yenye maadili, nampongeza kwa kuitwa mama na akumbuke kwamba mafunzo yake kwa mtoto wakati wa malezi ndio nguzo kwa mtoto ukubwani. Sipati picha maisha yangekuwaje bila wanawake, fikiria na wewe alafu naamini utajifunza umuhimu wa wanawake duniani.

Leo natoa dedication ya wimbo wa “power of the women” kwa wanawake wote wanao itwa Grace au Neema maana majina hayo yamebeba historia kubwa sana kwangu. Awe ni bibi, mama, dada, mke, mchepuko ama binti yote hayo ni majini lakini yanasimama kwa wanawake. Nawapenda sana na Mungu azidi kuwapa nguvu katika kutimiza majukumu yenu.

Poor Makonda…! by Chege Kalahala

Chege Kilahala

In politics, don’t ever let your opponents have a chance “to define” you before you have defined yourself. Thats why politicians in the western world like to write books about their life stories. It gives them a chance to “set the records straight” before their political opponents hijack their stories and paint them however they see fit.

Considering his background, Makonda should have dealt with his past a while ago……! And he still can……..

Mh. Paul Makonda

He has a personal story to tell….of a guy who…despite many obstacles….swam against the tide to reach where he is…..a story that can resonate with a lot of aspiring young men and women…..from all those failures in school and yet be able to pick up yourself and get going…..thats inspiring….! Of course, he will have to start by admitting his blunder and failure to be honest with Tanzanians upfront……My wish is that, there were good PR (public relations) experts in Tanzania….

Well….what can we do?!

JUKWAA LA WATU WENYE ULEMAVU TANZANIA-na Peter Sarungi

Na Peter Sarungi (The next Speaker)

 Nitumie fursa hii kutoa shukurani kwa wote walio jitolea na hata kufuatilia kwa karibu juu ya uundwaji wa Jukwaa la Watu wenye Ulemavu Tanzania. Mpaka sasa tumekamilisha 95% ya taratibu za kusajili Taasisi hii muhimu kwa walemavu. Jamii ya watu wenye ulemavu imeendelea kutengwa katika mipango mbalimbali ya kijamii, kisiasa na kiuchumi kwa sababu ya kukaa kimya bila kusema juu ya changamoto zetu, uwezo wetu, vikwazo tunavyokumbana navyo na hata mafanikio yetu. Ni muda sasa umefika wa kusema kwa nia ya kutetea na kushawishi maswala ya watu wenye ulemavu Tanzania ili na sisi Tanzania tufanane na wenzetu wa Afrika Mashariki walio amua kutekeleza kwa maneno na vitendo mkataba wa UN unao husu jamii ya walemavu na ni mkataba ambao Mh. Mkapa aliridhia na kusaini kisha Mh. Kikwete kuruhusu utungwaji wa sera na sheria no.9 ya watu wenye ulemavu na sasa kilichobaki ni kupiga kelele juu ya utekelezaji wake.

Ni jukumu letu sote kupiga kelele tena bila utengano na kwa sauti moja hata kama wewe sio mtu mwenye ulemavu lakini ukiguswa na hili basi ni sahihi kusema kwa nguvu hadi jamii, serikali na wadau wengine wapate kusikia ujumbe huu. Kuna msemo unasema hivi…

“Mtoto anayelia na kupiga kelele sana ndiye anaye pewa nyonyo na mama yake, ukinyamaza maana yake umeshiba”

Sidhani kama sisi watu wenye ulemavu tumeshiba katika nchi yetu, la hasha ila tuna ugulia kimya huku tukifa na tai shigoni. Ukimya wetu ndio unao tufunga, unao turudisha nyuma, unao tififisha ndoto zetu, unao tukosesha thamani na ndio sababu ya kutengwa na fursa.

Tanzania amka useme jambo kwa jamii hii ili na wewe ushiriki katika kutetea na kushawishi maswala ya watu wenye ulemavu Tanzania.

“Women are everywhere but Queens are scarce”!

“hardcore truth”!

Hardcore Truth!  Huwezi kuoa au kutembea na warembo wote, wanawake wazuri siku zote wataendelea kuwepo, kila siku utakutana nao wapya. jifunze kuwa na adabu (self discpline) pamoja na kujidhibiti (self control).

Chagua mmoja tu, mjenge awe wako, mfanye awe malikia wako! hii itakupunguzia gharama, itakutunzia muda wako, drama pamoja na magonjwa.

Vile vile hakuna medali, tuzo au nishani ya juu ya ushindi wa kuwa na wanawake wengi, bali ni kuzifungia baraka ambazo Mungu anataka kukupa na kujipeleka mwenyewe kaburini mapema. Jiongeze brother!

Busara yangu; A realman sees no other females becoz he only has eyes for his girl! Mwl Tweve Hezron.

2017-Hottest And Best Couple Of The Year!

Mr and Mrs Joseph Musira ndio Hottest And Best Couple of the Year!……Sababu haswa ya kuichagua hii couple kwanza nimeamua kwa mwaka huu ni enzi wazee wetu. Pili miaka 53 ya ndoa si kitu kidogo lazima kiheshimiwe! Napia ni kwasababu wanastahili!!……Basi ifuatayo ni historia yao fupi ambayo nitaieleza kwa kutumia picha zao za sherehe ya miaka 50 ya ndoa yao (Golden Jubilee of their wedding) ambayo ilifanyika huko Musoma, Mara miaka 3 iliyopita! Sherehe hiyo ilianzia kanisani ambapo walibariki ndoa yao na kuvaa pete ya nadhiri ya miaka hamsini!…….Haya furahia picha and Happy Valentine’s Day to you all! Maombi na kiapo yakiendelea ……….. Mr Joseph Musira na Felister Awiti wao ni wazaliwa wa mkoa wa Mara. Walikutana kwa katika kijiji kimoja kijulikanacho kama Kowak katika wilaya ya Rorya mkoani Mara. Felister yeye ni mzaliwa wa kijiji hicho cha Kowak akiwa ni mtoto wa kwanza wa mzee Cornel Awiti. Wakivishana pete baada ya ndoa kubarikiwa!…….Mzee Joseph Musira yeye ni Mwalimu kwa taaluma; hivyo wakati alipokutana na Felister alikuwa ni Mwalimu wa Kowak Middle School ambayo ipo chini ya missionary ya Wakatoliki. Kwasasa shule hiyo imebadilishwa na kuwa secondary ya wasichana ijulikanao kama Kowak Girls Secondary School ambayo mimi nilikuwa ni miongoni mwa wanafunzi walio fungua shule hiyo kwa mara ya kwanza. Mdogo wangu anaye nifuata kuzaliwa naye alisoma hapo! Picha ya pamoja na viongozi wa Diocese ya Musoma ambapo mzee Musira amekuwa mtumishi wao mpaka leo hii! Alianza kwa kufundisha kama Mwalimu, baadaye alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa shule zote za mkoa wa Mara ambazo zinamilikiwa na kanisa Katoliki mkoani humo! Ali stahafu akiwa katika cheo hicho zaidi ya miaka 5 iliyopita, lakini kwa uwadilifu wake na maadili mema kazini walimuomba kuongoza charity organization ambayo ipo chini la kanisa hilo hapo Mwembeni street, Musoma. 

Cheti kiki kabidhiwa toka Vatican kwa Papa!….. Furaha iliyoje! Wakielekea ukumbini kwenye sherehe!…..Kama nilivyo waeleza hapo mwanzo kuwa Mzee Musira alikutana na bibi Felister katika kijiji cha Kowak akiwa Mwalimu. Basi naye bibi Felister alikuwa ni Registered Nurse katika hospitali ya Kowak Mission ambayo nayo ipo chini ya missionary ya Wakatoliki. Ambapo pia baba yake mzazi bibi Felister alikuwa akifanya kazi kama Clinical officer katika hospitali hiyo…….Miaka miwili baada ya wapenzi hawa kukutana waliamua kufunga ndoa, kula kiapo kitakatifu mbele za Mungu na uso wa dunia! Hapo ilikuwa tarehe 12 / September / 1964! Kama mnavyo jua kuwa maswala ya kuoa katika familia za Kiafrika si kitu cha mchezo kama wenzetu wa dunia ya Magharibi ambapo wapenzi wanaweza kuwataharifu wazazi wao kupitia Facebook, text msg, Tweeter, na Instagram kuwa wao wamepanga kuoana siku fulani na wazazi wakafurahia kabisa kwa furaha kuu! Hapana, ndoa ni agano takatifu lazima liheshiwe sana kwa kufata taratibu maalum za kimila na kidini! Basi ndivyo hivyo kama wafanyavyo wengine naye alifanya! Mzee Musira alifata mila za Waluo ili kuweza kumchumbia na kumuoa bibi Felister! Yeye aliambiwa atoe mahali ya ng’ombe 12 na pia amjengee mama nkwe nyumba ya mabati ya vyumba vitatu na sebule! Awwwh! Huu ukoo wa Awiti siyo watu wa sport sport ati 🙂 🙂 🙂  Si mnajua kuwa bibi Felister alikuwa msomi (Registered Nurse) wa nguvu 🙂 🙂 hivyo baba mtu hakutaka mchezo na binti yake! …….Ukisikia “mapenzi mubashara” basi haya ndo yenyewe kwani mzee Musira alitekeleza hayo masharti yote bila pingamizi! Hiyo nyumba ndio mama mkwe wake aliishi mpaka mauti ilipo mkuta mwaka 2014! Tutakiane mkono wa amani mpenzi wangu, tumetoka mbali sana. Asante sana kwa “mapenzi mubashara”…..,hayo yalikuwa maneno matamu kabisa kutoka kwa mzee Musira kwenda kwa la azizi wake bibi Felister ???   Champaign zikifunguliwa na watu wenye nyuso za furaha kabisa! Aliye vaa vazi la kitenge ni mdogo wake bibi Felister aitwaye Anna Cornel au Mrs Obure. Yeye ndiye anaye mfuatia Felister, ni Mwalimu mstahafu hapo Musoma. Baada ya kufunga ndoa bibi Felister ilibidi ahame kwenye nyumba aliyopewa kuishi kama nurse mkuu hapo mission na pia alibadili jina lake la mwisho kutoka Awiti kwenda Musira. Hapo ndipo walifanya maamuzi ya kuhamia Musoma, na miezi michache baadaye mzee Musira alipelekwa Germany kuongezea utaalamu zaidi katika fani yake! …….Waliishi Musoma kwa miaka kadhaa na baadaye mwaka wa 1970 waliamishiwa Moshi ambapo waliishi kwa zaidi ya miaka 10 kabla ya kurudishwa tena Musoma……. Mr na Mrs Musira wao wamebarikiwa kupata watoto 6. Watatu wa kiume (Musira, Gerald, na Peter) na watatu wakike (Eddina, Yasinter, na Neema). Eddina a.k.a Eddi yeye ndio mtoto wa kwanza na Neema ndio wa mwisho! Kwa bahati mbaya kijana wao aitwaye Peter yeye alisha lala usingizi wa mauti; hivyo hayupo nao tena! May his soul continue to rest in peace!Mungu pia amewajalia kupata wajukuu wanne! Wakiume watatu na wa kike mmoja!  Wakinyweshana kinywaji maalum cha siku hiyo Mahaba mahabani! Kama walivyo shikamana siku ya kwanza pale Kowak basi ndivyo watakavyo shikana mikono yao mpaka mauti itakapo watenganisha! Waki kata keki kwa upendo na furaha Nilishe nikulishe ndio ishara ya upendo Mungu ni pendo. Penye Mungu kuna upendo mwingi na furaha isiyo elezeka! Hapa siongelei tu ndoa za “maigizo”, zile ndoa za ku-show off picha kwenye mitandao ya kijamii wakati ndani ya nyumba zenu wengine hawahemi! hapana! Naongelea real marriage, real commitment, honoring your vowels!!………. Miaka 53 ya ndoa hakuna michepuko wala mtoto wa “bandia”! Jamani, inawezekana!! These are real people in our communities; nina huwakika wapo wengine wengi tu!………Ee Mwenyezi Mungu endelea kumimina baraka zako kwenye hii ndoa na familia yao, Amen!

Couples we like!

Je, upo tayari?! Couple yangu ya pili -2016

Are you ready!!! Hii ndio ilikuwa couple yangu ya pili kuichagua. Mpaka sasa sijajutia kuichagua. Yani couple zote bado zipo kwenye mahaba mazito sana!! Nawaombea Mungu ndoa zao zidumu milele na awatangulie katika kila jambo! Kama ulipitwa soma HottestAndBestCouple-2016 …….. Je, upo tayari kwa 2017?!! Stay tuned!

je, upo tayari?! Couple yangu ya kwanza -2015

Nilipo anza ku-blog ilikuwa ni mwezi wa Pili mwaka 2015. Na hii ndio ilikuwa couple yangu ya kwanza kabisa kuichagua kama Hottest and Best Couple of the yr kwa mwaka huo! Nikitu niliamua kufanya kila tarehe 14/2 ya mwaka (siku ya Valentine day) nitatangaza couple moja iliyonivutia ambayo pia naona kuwa ni mfano mzuri wa kuigwa katika jamii! Kama ulipitwa na tangazo hilo tazama hapa ? HottestAndBestCouple-2015

Je, upo tayari kwa mwaka huu?? Stay tuned!!

TAIFA LA JANA, LEO NA KESHO…. na Peter Sarungi

Imeandikwa….

1. Baba bora ni yule anayelinda na kutetea familia yake, anaye tengeneza urithi mzuri kwa watoto, wajukuu hadi vitukuu na anaye hashimu familia yake.

2. Mke mwema ni yule anaye jenga familia yake bila kuharibu kwa mikono yake, anaye lea watoto katika maadili mema na anaye simama imara na mumewe katika hali ya hatari, dhiki, shida, raha, hofu, furaha, matatizo kama ya siasa, umasikini, chuki, wakati wa ujana na uzee, wakati wa afya na magonjwa.

3. Mtoto bora ni yule anaye heshimu wazazi wake na kujifunza maadili na maarifa kutoka kwa walio mtangulia. Ambaye anapenda kuwa kichwa na si mkia. 

Na Peter Sarungi (Next Speaker)

#MyTake.

Vijana ambao wamefika umri wa kujenga familia wachukue hatua kufanya hivyo, wasisubiri harusi na madoido ya kifahari maana kuna maisha ya ndoa baada ya kupata sifa za harusi.

??Fidel Pilato alikuwa akiangalia post zangu  za nyuma huku akijaribu kuuliza maswali katika lugha nisiyo tambua.???…Hao ndio watu wazima wadogo, Taifa la kesho. NIWATAKIE MWANZO MZURI WA WIKI………MUNGU BARIKI KAZI YA MIKONO/AKILI ZENU.

Ubaguzi wa watu wenye ulemavu nani alaumiwe na nini kifanyike?!

Hongera sana shule direct kwa jitihada zenu za kuokoa maisha ya watoto katika nyanja ya elimu!……Binafsi najiuliza hivi nani wakulaumiwa na nini kifanyike juu ya watu wenye ulemavu?! Mimi nasema ni ubaguzi wa wazi wazi kwa watu hawa na jamii imelifumbia macho! …….Miaka ya nyuma tulisema kuwa watu hawana uwelewa na leo hii je tunasemaje?! Shule moja ya secondary ya viziwi tena ni private?! Majengo mengi yanajengwa bila kujali kuwa tunao walemavu katika jamii yetu!! Majengo na maeneo mengi hakuna parking za magari specific kwa walemavu! Makanisa mengi sana hayana wakalimani wa viziwi! n.k………Huu ubaguzi ni mpaka lini? Nani wakulaumiwa? Na nini kifanyike? ……..Tafakari na chukua hatua!

Katika kuitafuta furaha usimuumize mtu mwingine ili wewe uwe na furaha- Dina Marios

Katika kuitafuta furaha usimuumize mtu mwingine ili wewe uwe na furaha.Kila lililopangwa kuja kwako litakuja tu kama Mungu amelipanga kuja.  Huwa nayatazama maua yakiwa bustanini.Ni maua ya aina tofauti lakini hupokezana kuchanua.Hili litakaa miezi hata tisa bila kuchanua lakini siku likichanua linapendeza kweli kweli,lingine huwa limechanua mara zote,lingine huitaji jua kali ili lichanue na kupendeza.Ndivyo hata sisi tulivyo hatufanani na kila mmoja ana wakati wake wa kuchanua…wakati wake wa kufanikiwa.Sidhani kama yale maua huwa yanaoneana wivu mbona yule kachanua mimi sijachanua?Usiitazame furaha ya mwenzako ukateseka nayo,mafanikio yake ukateseka nayo na wewe ukaitaka pengine na yeye ni kama lile ua linalokaa miezi tisa ndio lichanue.Itazame safari yako na wewe wakati wako ukifika utachanua Utang’ara.

Katika  kuitafuta furaha na mafanikio njiani usimkanyage mtu,usimuumize mtu.Unaweza kufanikiwa leo lakini sio milele.Kufumba na kufumbua mambo yanaweza kubadilika.Unaweza kuwa kwenye nguvu na control leo lakini huwezi kuushinda muda…muda hubadilika….Good morning!